Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 25 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 209 2021-05-07

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWEL X. HHAYUMA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara ya Kondoa – Gisambalang – Nangwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Samwel Xaday Hhyuma, Mbunge wa Hanang’, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Kondoa - Nunguri - Mtiriyangwe - Gisambalang - Nangwa yenye urefu wa kilometa 81.4 ni barabara inayosimamiwa na Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara nchini TANROADS baada ya kupanda hadhi mwaka 2010 kutoka barabara ya wilaya na kuwa barabara ya mkoa.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kutambua umuhimu wa barabara hii, imekuwa ikitenga fedha kwa ajili ya matengenezo mbalimbali ya ukarabati ili ipitike kwa mwaka mzima. Katika mwaka wa fedha huu 2020/2021, barabara hii ilitengewa jumla ya milioni 888.8 kwa ajili ya matengenezo mbalimbali na ukarabati na Shilingi milioni 60 kwa ajili ya usanifu wa Daraja la Mungurwi. Serikali itaiweka barabara hii katika mpango wa kuijenga kwa kiwango cha lami kulingana na upatikanaji wa fedha. Hata hivyo, Serikali itaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hii kuhakikisha kuwa inapitika vizuri majira yote ya mwaka. Ahsante.