Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia maji wananchi walio katika Vijiji ambavyo havifikiwi na Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria katika Jimbo la Tabora Kaskazini?

Supplementary Question 1

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli sijapata majibu mazuri namna hii katika Serikali hii ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, namshukuru sana. Nawapongeza sana Wizara ya Maji. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo nina maswali madogo tu mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa vile vijiji vitano alivyovitaja Ikongolo, Kanyenye, Kiwembe, Kongo na Hurumbiti ni bakaa ya mradi wa Ziwa Viktoria na hela zake zipo shilingi bilioni 25. Je, lini mradi huu wa kumalizia vijiji hivyo vitano utaanza?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa vile wananchi wangu wa Jimbo la Tabora Kaskazini wanahitaji mafunzo na elimu kuhusu matumizi ya maji hayo, lakini vilevile kuhusu utunzaji wa miundombinu ya maji, je, lini elimu hiyo kwa wananchi itaanza kutolewa? Ahsante sana.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge Mzee wangu Almas Maige kwa kazi kubwa na nzuri hasa ya kuwapigania wananchi wake wa Tabora kuhakikisha maji tunayatoa Ziwa Viktoria na kuyapeleka Tabora, Igunga, Nzega. Historia itakukumbuka mzee wangu, Mungu akubariki sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake kwamba lini tutatekeleza mradi katika vijiji vitano, nataka nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge, sisi Wizara ya Maji si Wizara ya Ukame, vijiji vile vitano vilivyobaki tunakwenda kuvikamilisha mara moja ili wananchi waweze kupata huduma ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kubwa kuhusu suala zima la elimu katika eneo lile la Tabora, Wizara ya Maji tumetekeleza mradi mkubwa sana wa zaidi ya bilioni 600 katika Mji wa Tabora, Igunga, Nzega. Pasipo elimu kwa wananchi inawezekana wakahujumu miundombinu ya maji. Hii ni kazi yetu sote Mheshimiwa Mbunge, mimi Waziri wa Maji na Waheshimiwa Wabunge wote kuhakikisha kwamba tunatoa elimu ya kulinda na kutunza vyanzo na miundombinu ya maji ili kuhakikisha wananchi hawa wanaenda kuvilinda na kuvitunza, ili miradi hiyo iwe na manufaa kwa vizazi vya sasa na vya baadaye. Ahsante sana.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia maji wananchi walio katika Vijiji ambavyo havifikiwi na Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria katika Jimbo la Tabora Kaskazini?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Napenda kuuliza swali langu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na jitihada kubwa zinazofanywa na Wizara ya Maji kusambaza maji zinaweza kuwa bure kama gharama za kuunganisha maji hazitashushwa. Swali langu ni hili, kwa nini Serikali isishushe gharama za kuunganisha maji, ikiwa ni pamoja na kuzuia wananchi kulazimishwa kununua vifaa vya kuunganisha maji kwenye Mamlaka za Maji na gharama zake zikawa kama umeme wa REA shilingi 27,000? Ahsante.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge. Sisi kama Wizara ya Maji jukumu letu ni kuhakikisha Watanzania wanapata huduma ya maji, si maji tu, lakini kwa gharama nafuu. Kwa hiyo, nikiwa Waziri wa Maji tumepokea ushauri, ahsante sana.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia maji wananchi walio katika Vijiji ambavyo havifikiwi na Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria katika Jimbo la Tabora Kaskazini?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Mji wa Munze katika Wilaya ya Kishapu ni mji ambao umepata maji ya Ziwa Viktoria. Kumekuwepo na tatizo kubwa sana la maji kukatika katika Mji wetu wa Kishapu, wa Munze. Je, ni tatizo gani linalosababisha maji haya kukatika huku tukitambua kwamba maji ya Ziwa Viktoria yamekuwepo kwa wingi sana na halipo tatizo la maji, lakini changamoto kubwa ni kukatika kwa haya maji? Naomba majibu.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Kishapu kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tuna mradi ambao tumepeleka maji ya Ziwa Viktoria katika Jimbo lake la Kishapu. Kukatika kwa haya maji changamoto kubwa ilikuwa ni deni la umeme. Sisi kama Wizara ya Maji tumeshatoa milioni 600 kuwapa wenzetu wa KASHWASA kuhakikisha wanalipa deni lile TANESCO ili wananchi waendelee kupata huduma ya maji safi na salama. Ahsante sana.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia maji wananchi walio katika Vijiji ambavyo havifikiwi na Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria katika Jimbo la Tabora Kaskazini?

Supplementary Question 4

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa kuwa Wizara ya Maji ina dhamira njema na wananchi wa Jimbo langu la Manyoni Magharibi. Kuna visima ambavyo vimeahidiwa na Wizara katika Vijiji vya Jeje, Njirii, Kamenyanga, Itagata, Ukimbu, Chabutwa, Makale na Kalangali na Itagata, je, ni lini wataenda kuchimba visima hivi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya. Kubwa nimuombe Mheshimiwa Mbunge baada ya dakika chache nakuja kuwasilisha bajeti yangu ya Wizara ya Maji na bajeti yetu imesikiliza ushauri wa Waheshimiwa Wabunge. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge tumezingatia maelekezo yako katika kuhakikisha wananchi wako tunawachimbia visima. Ahsante sana.

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia maji wananchi walio katika Vijiji ambavyo havifikiwi na Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria katika Jimbo la Tabora Kaskazini?

Supplementary Question 5

MHE. AGNESTA L. KAIZA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Pamoja na utoaji na usambazwaji wa maji mijini na vijijini bado kuna malalamiko makubwa sana ya ankara za maji kutokuwa na uhalisia. Je, Serikali ina nini la kusema au kuna tamko gani la Serikali ili kuondoa mkanganyiko huu ambapo wananchi wanabambikwa ankara ambazo hazina uhalisia? Ahsante sana.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote nimshukuru Mheshimiwa Mbunge lakini niseme tu wazi ni haki ya mwananchi kupatiwa huduma ya maji na mwananchi ana wajibu wa kulipia bili za maji, lakini wajibu huo wa kulipia bili za maji zisiwe bambikizi. Kwa hiyo, maelekezo ya Wizara yetu ya Maji kwa Mamlaka zote za Maji nchini watoe bili halisia ambazo zimeidhinishwa na EWURA. Ikiwa kuna Mkurugenzi au msoma mita kwa makusudi anambakizia mwananchi bili ya maji tutashughulika naye.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia maji wananchi walio katika Vijiji ambavyo havifikiwi na Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria katika Jimbo la Tabora Kaskazini?

Supplementary Question 6

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Kwanza nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa juhudi zinazoendelea za kuwapatia maji wananchi wa Jimbo la Kyerwa kwenye Mradi wa Vijiji 57.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini ziko kata ambazo haziko kwenye Mradi wa Vijiji 57, kama Kata ya Bugara, Kibale, Businde pamoja na Mlongo. Nini juhudi za Serikali kuwapatia wananchi hawa maji?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nampongeza sana sana kaka yangu Mheshimiwa Bilakwate kwa kazi kubwa na nzuri anayoifanya katika Jimbo lake la Kyerwa. Kubwa ambalo nataka kusema, sisi kama Wizara ya Maji, tumejipanga na zaidi ya miradi 1,527 tunakwenda kuitekeleza katika maeneo ya vijijini katika kuhakikisha wanapata huduma ya maji.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimhakikishe maeneo ambayo hayana maji, sisi kama Wizara tumejipanga kuhakikisha tunawafikishia hii huduma ya maji safi na salama.