Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 24 Water and Irrigation Wizara ya Maji 203 2021-05-06

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwapatia maji wananchi walio katika Vijiji ambavyo havifikiwi na Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria katika Jimbo la Tabora Kaskazini?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Almas Athuman Maige, Mbunge wa Tabora Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Tabora Kaskazini lina kata 19 na vijiji 82. Katika utekelezaji wa mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kwenda katika Miji ya Nzega, Igunga na Tabora jumla ya vijiji 20 vya Jimbo la Tabora Kaskazini ambavyo ni Ibushi, Igoko, Isikizya, Ikonola, Ikonola, Mswa, Itobela, Ibelamilundi, Isenegezya, Mtakuja, Majengo, Kalemela, Saw Mill, Imalampaka, Magiri, Kinyamwe, Lunguya, Upuge, Kasenga na Mhogwe vimenufaika na mradi. Aidha, Serikali imekamilisha utekelezaji wa miradi mitatu ya mtandao wa bomba inayonufaisha vijiji vinne vya Kilungu, Milumba, Migungumalo na Ishihimulwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2020/2021, Serikali iko kwenye hatua za awali za utekelezaji wa miradi sita itakayonufaisha vijiji kumi na mbili vya Makazi, Ugowola, Ndono, Mbiti, Kalola, Ufuluma, Nzubuka, Izugawima, Ibiri, Mayombo, Nsimbo na Kagera. Katika Mpango wa bajeti ya fedha 2021/2022, Serikali imepanga kutekeleza miradi mitano itakayonufaisha vijiji vinane vya Ikongolo, Kanyenye, Kiwembe, Kongo na miji 28 kwa gharama ya Dola za Marekani milioni 500 kutoka Benki ya Exim India ambao utanufaisha vijiji 14 na hivyo kufanya jumla ya vijiji 58 vya Jimbo la Tabora Kaskazini kupata huduma ya maji.