Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kiwanja cha Ndege cha Mwada Mkoani Manyara?

Supplementary Question 1

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi uliyonipa ili niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, Mkoa wetu wa Manyara ni miongoni mwa mikoa yenye vivutio vingi kama vile Hifadhi ya Wanyama Tarangile, tuna Mlima Hanang, tuna Ziwa Babati. Kutokana na ukosefu wa Kiwanja cha Ndege katika mkoa wetu watalii wengi wanapokuja katika mkoa wetu hutumia Uwanja wa Ndege uliopo Manyara kule Mto wa Mbu umbali wa kilometa 160, hutumia Uwanja wa Ndege uliopo KIA kilometa takribani 200, hutumia Uwanja wa Ndege wa Arusha kilometa zaidi 164. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, je, Serikali haiwezi sasa kuweka msukumo wa pekee kusogeza huduma ya Uwanja wa Ndege katika Mkoa huu wa Manyara ili kuchochea shughuli za maendeleo katika mkoa wetu? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa tayari eneo hili limekwishatengwa kule Mwada, ni lini sasa Serikali itaona kuboresha ili kuweka airstrip katika eneo hilo litumike wakati tunaendelea kusubiri ujenzi wa Uwanja wa Ndege katika mkoa wetu? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Regina Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Manyara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kufanya kazi za kibunge wa Mkoa, kwa sababu nina uhakika uwanja huo ukijengwa na kukamilika huduma itakuwa ya mkoa na mikoa ya jirani. La pili naomba nimuhakikishie kwamba jambo hili Mheshimiwa Pauline Gekul Mbunge wa Babati Mjini na wengine wenye majimbo wamekuwa wakifuatilia kwa muda mrefu.

Mheshimiwa Spika, majibu ya Serikali ni kwamba tuna- engage Mkandarasi Mshauri tuelekeze fedha katika eneo hili, tunajua umuhimu wake na vitu vyote katika Mkoa wa Manyara ukamilike.

Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali lake la pili linalohusu wazo lake la kutengeneza airstrip katika eneo hili, tunalipokea na tutalifanyia kazi ili huduma iweze kupatikana katika eneo hilo. Ahsante.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kiwanja cha Ndege cha Mwada Mkoani Manyara?

Supplementary Question 2

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa nafasi hii. Takwimu mbalimbali za wataalam zimeonesha kama Uwanja wa Ndege wa Serengeti ukiboreshwa utakuwa uwanja pekee katika Kanda ya Ziwa utakaoleta tija kubwa kiuchumi, kiuhifadhi na kijamii kwa wananchi wa Serengeti na Tanzania kwa ujumla. Kwa kuwa mpaka sasa tayari wadau mbalimbali na wananchi wamekwishachangia ujenzi wa uwanja huu. Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kufanikisha ujenzi wa uwanja huu?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Serengeti, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza ni kweli Uwanja wa Serengeti ni muhimu sana kwa maendeleo ya kiuchumi ya nchi lakini pia katika eneo la Serengeti na Mkoa wa Mara kwa ujumla. Pia naomba nitambue kwamba ni kweli wananchi na Mheshimiwa Mbunge amejiunga, wametengeneza group la WhatsApp, wanachangisha fedha na Mheshimiwa Mbunge leo ameomba appointment watu wakija awapokee tuzungumze.

Mheshimiwa Spika, naomba nimwelekeze Mkurugenzi wa Viwanja vya Ndege atume watalaam wetu katika eneo hili ili juhudi nzuri za wananchi zisipotee, atuongezee utalaam wa Wizara yetu kazi hii ifanyike na uwanja ujengwe ili watalii wasizunguke Zaidi, washuke pale karibu na tutape huduma na fedha iongezeke.