Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 21 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 172 2021-05-03

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. REGINA N. QWARAY aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Kiwanja cha Ndege cha Mwada Mkoani Manyara?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Regina Ndege Qwaray, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Manyara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege yaani TAA na kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara wameainisha eneo la Mwada katika Halmashauri ya Wilaya ya Babati kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanja cha Ndege katika mkoa huo. Aidha, Serikali imeendelea na taratibu za kutwaa eneo hilo kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja hicho cha ndege. Baada ya hatua hii, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi yaani Sekta ya Ujenzi kupitia TANROADS, itatangaza zabuni ya kumpata Mshauri Mwelekezi wa kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

Mheshimiwa Spika, kwa maelezo hayo hapo juu, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa, Serikali ina nia thabiti na imejipanga kikamilifu katika kuhakikisha kuwa uwanja huo unajengwa ili kuweza kutoa huduma muhimu katika Mkoa huo wa Manyara na maeneo ya jirani. Ahsante.