Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji kwenye Mji wa Usagara?

Supplementary Question 1

MHE. ALEXANDER P. MNYETI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi hii. Majibu haya anayonipa Naibu Waziri wa Maji ni majibu ambayo yametolewa mwaka 2002 swali lilipoulizwa na Mheshimiwa Dalali Shibiliti, majibu hayo hayo; miaka kumi baadaye akauliza Mheshimiwa Charles Kitwanga akapewa majibu hayo hayo; nami nauliza miaka kumi baadaye napewa majibu haya haya.

Mheshimiwa Spika, nataka kujua, maji Usagara yanakwenda lini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mnyeti Mbunge wa Misungwi. Awali ya yote Mheshimiwa Mnyeti pamoja na wananchi wote wa Misungwi poleni sana kwa adha hii ambayo imewapata kwa muda mrefu. Mheshimiwa Mbunge kama anavyofahamu Awamu hii ya Sita, ni awamu ambayo inakwenda kumaliza kama sio kupunguza kwa sehemu kubwa tatizo la maji. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama tulivyomsikia Mheshimiwa Rais, yeye mwenyewe akiwa hapa ndani kwa kutumia Bunge lako hili Tukufu aliahidi kuweka nguvu kubwa ya kuona kwamba matatizo ya maji yanakwenda kutatuliwa. Hivyo kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi, kwenye bajeti yetu ya mwaka 2021/2022, tunakuja Misungwi kuhakikisha tatizo hili sasa linabaki kuwa historia. (Makofi)