Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 21 Water and Irrigation Wizara ya Maji 170 2021-05-03

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka maji kwenye Mji wa Usagara?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Alexander Pastory Mnyeti, Mbunge wa Misungwi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji Wilayani Misungwi ni asilimia 73. Katika juhudi za kuboresha upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi wa maeneo hayo, katika mwaka 2021/2022, Serikali kupitia Programu ya Lake Victoria Water and Sanitation imepanga kutekeleza mradi wa maji katika maeneo ya Usagara, Buswelu, Kisesa na Buhongwa. Mradi huu utahusisha ujenzi wa vituo vya kusukuma maji viwili, mifumo ya usafirishaji na usambazaji maji yatakayozalishwa na Chanzo kipya cha Maji Butimba, ulazaji wa mabomba makubwa yenye ukubwa wa kuanzia milimita 50 hadi 600 kwa umbali wa kilomita 50, ujenzi wa matanki manne ya ukubwa mbalimbali.

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi huo utanufaisha maeneo yote ya Mji wa Usagara ikiwemo Usagara, Fela, Nyang’homango, Idetemya, Ukiliguru, Ntende, Sanjo, Isamilo, Mayolwa, Bukumbi na Kigongo.