Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SIYLVESTRY F. KOKA aliuza:- Je, ni lini Serikali itaanza kumaliza mradi wa ujenzi wa barabara ya Makofia - Mlandizi - Vikumburu kupitia Mbwawa kwa kiwango cha lami ambayo ipo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi?

Supplementary Question 1

MHE. SIYLVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu haya ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, toka barabara ile ya njia nane kutoka Kimara hadi Kibaha kukaribia kukamilika kumekuwa na ongezeko kubwa sana la magari katika Mji wa Kibaha kiasi kwamba kutoka Kibaha Mjini mpaka pale Mlandizi kiasi cha kilometa 15 unaweza ukatumia hata masaa mawili na nusu wakati kuna barabara ya zamani kutoka pale Picha ya Ndege kupita Kongowe hadi Visiga ambayo ingelirekebishwa tu ingeweza kuondoa huu msongamano wakati mpango wa ujenzi unaendelea. (Makofi)

Swali la kwanza, je, ni lini sasa Serikali inakamilisha ujenzi/inajenga barabara ya njia nane kutoka Kibaha Mjini mpaka Mlandizi angalau kuondoa usumbufu huo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, barabara ya kuanzia pale TAMCO hadi Mapinga na kuanzia kwa Mathias hadi Msangani zinazojengwa kawa kiwango cha lami zinasuasua sana ujenzi wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, je, Serikali ina mpango gani wa kutoa fedha na kukamilisha ujenzi huo ili matunda mazuri ya kazi ya Serikali yaweze kupatikana kwa wananchi wa Kibaha Mjini?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Koka Mbunge wa Kibaha Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nielekeze Meneja na TANROADS Mkoa wa Pwani ahakikishe kwamba anaondoa changamoto zote ambazo amepelekea barabara hii ujenzi wake unasuasua na kama kuna changamoto ambazo ameshindwa kuchukua hatua basi Wizara ipo tayari kutoa ushirikiano ili jambo hili na barabara ijengwe kwa wakati na kiwango kinachotarajiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali lake la pili naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba changamoto ambazo ametoa hapa na msongamano wa magari tutauchukulia hatua, Serikali inafanya kazi hii na Mkandarasi yupo site Sasa kwa sababu tunaenda kwenye weekend hii naomba nimuhakikishe kwamba kabla ya Jumatatu atakuwa amepata majibu sahihi nini kinafanya barabara isuwesuwe iweze kurekebishwa mapema sana na hata jana nilipigiwa simu na Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Mapinduzi ambao leo tuna kazi maalum wakikwama barabarani.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimwelekeze Katibu Mkuu tunapojiandaa sasa muda mfupi ujao Wabunge wa Chama cha Mapinduzi kwenda kupiga kura za ndio za Mama Samia kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi, changamoto hizo kwa wajumbe wanaporudi kwenda makwao hasa Dar es salaam hasa na maeneo jirani ziwe zimekomesha mara moja ahsante sana. (Makofi)