Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 20 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 167 2021-04-30

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SIYLVESTRY F. KOKA aliuza:-

Je, ni lini Serikali itaanza kumaliza mradi wa ujenzi wa barabara ya Makofia - Mlandizi - Vikumburu kupitia Mbwawa kwa kiwango cha lami ambayo ipo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Siylvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Makofia – Mlandizi – Vikumburu yenye urefu wa kilometa 135.97 ni barabara ya mkoa inayounganisha Wilaya ya Bagamoyo, Kibaha na Kisarawe.

Mheshimiwa Naibu Spika, upembuzi yakinifu na usanifu wa kina pamoja na uhakiki wa mali zitakazoathiriwa na mradi kwa sehemu ya Makofia – Mlandizi – Maneromango yenye urefu wa kilometa 100 umekamilika. Kazi za ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara hii zitaanza kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati ujenzi kwa kiwango cha lami ukisubiri upatikanaji wa fedha, Wizara ya Ujenzi itaendelea kuihudumia barabara hii ili iweze kupitika majira yote ya mwaka. Katika mwaka wa fedha 2020/2021 jumla ya shilingi bilioni 1,524.07 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo mbalimbali. Ahsante.