Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdulaziz Mohamed Abood

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Mjini

Primary Question

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD aliuliza:- Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro ina tatizo kubwa la msongamano katika wodi ya akina mama ambao wamekuwa wakilala zaidi ya wawili kwenye kitanda kimoja; (a) Je, ni lini Serikali itaongeza wodi ya wazazi katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Morogoro? (b) Je, kwa nini Serikali isiboreshe baadhi ya zahanati kama Mafiga Sabasaba ili kuwa na uwezo wa kupokea kina mama wajawazito kujifungua na kupunguza msongamano katika hospitali ya rufaa ya Morogoro?

Supplementary Question 1

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD: Mheshimiwa Naibu Spika, nina maswali mawili ya nyongeza;
Swali la kwanza, zahanati ya Mafiga inahudumia kina mama wengi lakini haina madawa kwa ajili ya akina mama na pia haina ultra sound machine ya akina mama.
Je, lini Serikali itaipatia zahanati ya Mafiga vifaa hivi?
Swali la pili, hospitali ya Mkoa wa Morogoro ambayo ipo njia panda ya barabara ya Morogoro inayokwenda Mikoa mingine yote ya Bara na ajali nyingi zinatokea, lakini haina mashine ya X-Ray, mashine iliyopo sasa hivi haifanyi kazi vizuri.
Je, Serikali haioni kama kuna uharaka wa kuipatia hospitali ya Mkoa wa Morogoro mashine ya X-Ray?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika maeneo yangu ambayo nimetembelea ni Morogoro, na jambo ambalo nimeshuhudia pale ni kwamba kama Mheshimiwa Mbunge pale kwa kweli kwa kutumia, licha ya ushawishi wakati mwingine anatumia resources zake mwenyewe kwa ajili ya wananchi wake. Naomba nikuhakikishe kwamba katika hii zahanati ya Mafiga uliyoisema ambayo changamoto kubwa ni madawa pamoja na vifaa tiba especially ultra sound na nimesema katika maelezo yangu ya awali. Katika research tuliyofanya haraka haraka vitu vingine vingekuwa vinaweze kupatikana kwa ukaribu sana lakini tatizo kubwa tulilokuwa nalo mwanzo ni kutokana na ile management ya fedha zilizokuwa zinapatikana.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia idadi ya wanaofika katika zahanati ya Mafiga pale lakini collection ilikuwa ni changamoto kubwa sana. Ndiyo maana tulitoa maelekezo ya kutosha licha ya kufanya juhudi zingine za upatikanaji wa dawa na vifaa tiba, changamoto kubwa ni kwamba tukienda kukusanya mapato yetu vizuri ambayo katika njia moja au nyingine unakuta kwamba baada ya kutumia mifumo ya electronic, collection imeenda zaidi ya asilimia 800. Watu waliokuwa wanakusanya shilingi laki moja leo wanakusanya shilingi milioni moja, unaona kwamba jinsi gani pesa hizi zikikusanywa vizuri zitaenda kusaidia katika suala zima la madawa na vifaa tiba.
Kwa hiyo Mheshimiwa Abood naomba nikuambie ninakuhakikishia kabisa kwamba katika zahanati ya Mafiga mimi na wewe kwa sababu tumeshaahidi kwamba tutaenda Morogoro, hii ni sehemu ya kwanza kwenda kubaini kuwa tatizo la msingi ni nini, na tutafanyaje kuondoa tatizo la madawa, kwa sababu mwanzo watu hata mwongozo walikuwa hawaufuati, pesa hata zikikusanywa haziendi katika madawa na vifaa tiba, isipokuwa watu wanagawanya kwa per diem na vikao vingine visivyokuwa na maana yoyote.
Mheshimiwa Naibu Spika, hivyo nimhakikishie Mheshimiwa Abood kwamba, hapa tutafanya ukatabati mkubwa ili utendaji wa zahanati hii na nyinginezo zinafanya kazi vizuri kwa ajili ya wananchi wa Morogoro.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la hospitali ya Morogoro ni kweli na mimi nikuambie kwamba miongoni mwa field practical zangu wakati nilipokuwa Chuo Kikuu mwaka 1998, nilifanya research zangu pale na field practical nilifanyia pale Morogoro, naifahamu vizuri hospitali ya Mkoa wa Morogoro. Ni kweli inapokea wagonjwa wengi sana na wakati mwingine hata ajali zikitokea watu wengi ni sehemu ya kimbilio, wanaotoka Iringa, Dodoma na sehemu mbalimbali pale ni kimbilio. Tunajua X-Ray machine ipo lakini haifanyi kazi vuziri, tuna mpango mpana sasa hivi wa Serikali hasa kwa ajili ya hospitali zetu za Mikoa na hospitali zetu za Kanda. Mpango huo sasa kwa Serikali ya Tanzania kwa kushirikana na Serikali ya Uholanzi tutahakikisha kwamba tunapeleka vifaa tiba katika hospitali zetu za Kanda na hospitali za Mkoa. Ninaamini na hospitali yetu ya Mkoa wa Morogoro tutaipa kipaumbele kutokana na strategic area yake ya kijiografia, lazima tuipe nguvu wananchi wa Morogoro waweze kupata huduma, ili wanufaike na huduma njema ya Serikali yao ya Awamu ya Tano ambayo inafanya kazi kwa maslahi ya Watanzania.

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, kuhusu suala la uhaba wa dawa katika vituo vyetu vya afya, ningependa kuwafahamisha Waheshimiwa Wabunge kwamba tunapitia upya vigezo vya kugawa fedha za dawa. Kwa sababu kwa kweli tumeona hakuna uwazi, unakuta kituo kingine kina wananchi wengi lakini mgao wa dawa fedha ya dawa ni ndogo. Kwa hiyo, nataka kuwathibitishia Waheshimiwa Wabunge tunaangalia upya vigezo kama ni hospitali ya Mkoa wanatakiwa kupata shilingi ngapi na taarifa hizi tutazitoa kwa kila Mbunge ajue kituo chake cha afya kinapata shilingi ngapi, hospitali yake ya Wilaya inapata shilingi ngapi na hospitali ya Mkoa inapata shilingi ngapi. Kwa hiyo, tunataka kuwa wawazi zaidi katika mgao wa fedha za dawa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD aliuliza:- Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro ina tatizo kubwa la msongamano katika wodi ya akina mama ambao wamekuwa wakilala zaidi ya wawili kwenye kitanda kimoja; (a) Je, ni lini Serikali itaongeza wodi ya wazazi katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Morogoro? (b) Je, kwa nini Serikali isiboreshe baadhi ya zahanati kama Mafiga Sabasaba ili kuwa na uwezo wa kupokea kina mama wajawazito kujifungua na kupunguza msongamano katika hospitali ya rufaa ya Morogoro?

Supplementary Question 2

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kuniona.
Katika Hospitali yetu ya Wilaya ya Geita ambayo imepandishwa hadhi kuwa hospitali ya Mkoa kuna msongamano mkubwa sana wa watu kiasi kwamba kwa kweli changamoto ni kubwa sana. Ningependa hasa kujua kwa sababu tunatakiwa tujengewe Hospitali mpya ya Rufaa ya Mkoa.
Ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi rasmi katika hospitali ya Mkoa ambayo itakuwa ni Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la ujenzi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Mheshimiwa Bukwimba tulikuwa na Mheshimiwa Makamu wa Rais tulifungua hospitali ile ya Geita, kweli kuna msongamano mkubwa, na pale ni kipaumbele, nadhani mchakato wa Serikali tutafanya mambo haya kwa haraka kuangalia bajeti ya mwaka wa fedha unaokuja, tuweke mipango ya pamoja ya Kiwilaya na Kimkoa na mwisho wa siku tujenge hospitali yetu ya rufaa ya Mkoa wa Geita.