Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 46 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 390 2016-06-20

Name

Abdulaziz Mohamed Abood

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Mjini

Primary Question

MHE. ABDUL-AZIZ M. ABOOD aliuliza:-
Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro ina tatizo kubwa la msongamano katika wodi ya akina mama ambao wamekuwa wakilala zaidi ya wawili kwenye kitanda kimoja;
(a) Je, ni lini Serikali itaongeza wodi ya wazazi katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Morogoro?
(b) Je, kwa nini Serikali isiboreshe baadhi ya zahanati kama Mafiga Sabasaba ili kuwa na uwezo wa kupokea kina mama wajawazito kujifungua na kupunguza msongamano katika hospitali ya rufaa ya Morogoro?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdul-Azizi Abood Mbunge wa Morogoro Mjini lenye sehemu a na b kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, msongamano wa wagonjwa katika wodi ya wazazi ya hospitali ya Mkoa unatokana na kukosekana kwa hospitali ya Wilaya ya Morogoro. Ili kukabiliana na tatizo hilo Serikali imepanga kuanza ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Morogoro katika bajeti ya mwaka 2016/2017. Fedha zilizotengwa ni shilingi bilioni 2.5 ili kuanza ujenzi wa jengo la utawala na jengo la wagonjwa wa nje (OPD).
Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa Serikali ni kuimarisha kituo cha afya cha Mafiga ambacho tayari kimeanza kutoa huduma za mama wajawazito. Katika mwaka wa fedha 2015/2016 Halmashauri imepanga kutumia shilingi milioni 100 kwa ajili ya kujenga jengo la upasuaji na wodi. Vilevile, zimetengwa shilingi milioni 71 katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 kwa ajili ya upanuzi wa wodi ya wazazi katika zahanati ya kihonda. Hivyo, mpango wa Serikali ni kuimarisha huduma za wazazi katika zahanati na vituo vya afya ili kupunguza msongamano katika hospitali ya rufaa ya Morogoro.