Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:- Je, ni kwa nini Serikali haitumii risiti za kielektroniki inapotoza faini za kuingiza mifugo kwenye Hifadhi zilizopo Sikonge?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu ya Serikali ambayo yametolewa vizuri kwa ufasaha, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; sina tatizo na risiti za MNRT Portal, tatizo langu ni kwa nini mtozaji wa faini asipewe post maalum ili atoe risiti halali badala ya zile za kuandikwa kwa mkono?

Mheshmiwa spika, swali la pili, kwa nini Serikali isitoe mwongozo kwa halmashauri na WMAs zote ili fedha zilipwe kwenye control number maalum benki badala ya kubeba kwenye mabegi na kwenda kulipia porini? Ahsante sana.

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kakunda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza ameongelea ni kwa nini tusitoe risiti za kielektroniki badala ya kutoa risiti za mkono. Kama ambavyo nimejibu kwenye jibu langu la msingi ni kwamba miongozo yote ya sasa tunayofanya ni kwamba Serikali inapokea mapato ya aina yeyote ile kutumia risiti za EFD na kwa upande wa Maliasili na Utalii tunatumia hiyo MNRT Portal ambayo ndio tunayopokelea fedha kwa kutumia control number.

Mheshimiwa Spika, suala analoliongelea Mheshimiwa Mbunge ni kwenye hizi Jumuiya za Hifadhi ya Wanyamapori ambazo zinasimamiwa na Serikali za Mitaa kupitia halmashauri na tunazieleleza sasa halmashauri kwa kuwa fedha zake za jumuiya hizi zinakaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali waangalie sasa utaratibu wa kuhakikisha kwamba malipo yote yanayotokana na faini yapitie kwenye utaratibu wa Serikali yaani EFD.

Mheshimiwa Spika, kwenye upande wa mwongozo, mwongozo tulishautoa na utekelezaji wake unaendelea kufanyika isipokuwa usimamizi tu kama ambavyo amesema Mheshimiwa Mbunge kwamba imeonekana kuna wananchi wanabeba fedha kwenye mifuko. Tunatoa maelekezo sasa kwa halmashauri ambazo zinasimamia hizi jumuiya kuhakikisha kwamba usimamizi wa fedha za Serikali unapitia kwenye mifumo ya TEHAMA iliyoainishwa na Serikali, ambayo kwa Maliasili na Utalii tunatumia MNRT Portal ambayo inakusanya kwa kutoa control number na kwa wale wanaotumia EFD, basi Halmashauri zisimamie suala hilo ili fedha hizi sasa ziweze kufika kwenye Mifuko husika na ubadhilifu usiweze kujitokeza. Naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:- Je, ni kwa nini Serikali haitumii risiti za kielektroniki inapotoza faini za kuingiza mifugo kwenye Hifadhi zilizopo Sikonge?

Supplementary Question 2

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa tatizo la mifugo kuingia katika hifadhi za Sikonge linafanana kabisa na tatizo lililopo katika Wilaya ya Namtumbo kwenye eneo la Hifadhi ya Selous au sasa hivi Mwalimu Nyerere, mifugo mingi iliyofukuzwa kutoka Morogoro imeingia katika hifadhi hiyo na kuharibu ecology ya tembo na sasa tembo wamekuwa wanakuja katika vijiji wanapoishi wananchi na jana wameuwa Imam wa Msikiti katika Kijiji cha Luhangano, Kata ya Mputa, Je, Serikali itafanya nini kuondoa mifugo hiyo na kutuletea askari wakae kule moja kwa moja kuzuia tembo kuleta madhara ya vifo kama yaliyotolea jana?

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Answer

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Kawawa kwa kazi nzuri anayowafanya wananchi wa Jimbo la Namtumbo.

Mheshimiwa Spika, ni kweli tumekuwa na changamoto ya mifugo kuingia katika hifadhi ambayo inasukuma wanyamapori wakiwemo tembo kuja sasa kwenye maeneo ya wananchi. Tunaendelea na operation ya kuondoa mifugo hiyo na kuwarudisha tembo katika maeneo yao stahiki. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, operations zinaendelea jana tu tumefanya operation katika Wilaya ya Tunduru na msiba anaosema katika Kijiji cha Mputa tayari Maafisa Wanyamapori watawa wapo Mputa hivi sasa kushughulikia suala hilo. Naomba kuwasilisha. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:- Je, ni kwa nini Serikali haitumii risiti za kielektroniki inapotoza faini za kuingiza mifugo kwenye Hifadhi zilizopo Sikonge?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kumekuwa na double standard, mifugo inapoingia hifadhini sio tu wanatozwa fidia na wengine ni fidia kubwa na hata wale wafugaji wamekuwa wakipata mateso, lakini tembo wanapokwenda kuharibu mazao ya wananchi na nyumba za wananchi fidia yake ni kidogo, hususan wananchi wa Serengeti, Wananchi wa Tamau, wananchi wa Nyamatoke, Wananchi wa Kunzugu wote hao wapo kando kando ya Hifadhi ya Mbuga Serengeti. Je, ni lini sasa Serikali itarekebisha fidia ya tembo wanapoharibu mazao au mali za wananchi ili iendane na hali halisi kuliko ilivyo hivi sasa fidia ya Shilingi 100,000/=. (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester Bulaya, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru sana Mbunge wa Viti Maalum Ester Bulaya kwa swali lake zuri.ni kweli kumekuwa na changamoto hii ya kwamba wafugaji wanatozwa fedha kubwa kwa maana ya kiwango ambacho kimewekwa kwenye sheria zetu hizi lakini inapokuja kwa mwananchi inaonekana kwamba Serikali haioni umuhimu.

Mheshimiwa Spika, lakini nimtoe wasi wasi Mheshimiwa Esther kwamba sisi tunachofanya ni kukemea uingizaji wa mifugo kwenye hifadhi na niwaombe wananchi ambao wanaishi kwenye maeneo ya pembezoni mwa hifadhi tembo hawa wanaangalia ni nini ulichopanda kwenye maeneo hayo na tunawahamasisha wananchi wapande pilipili lakini pia waweke mizinga ya nyuki.

Mheshimiwa Spika, nasema hivyo hawa tembo na Wanyama wengine wana Serikali yao na Serikali yao hii na wenyewe wanajadili kama ambavyo tunajadili sisi hapa. Na ukumbuke maeneo mengi ambayo ni ushoroba wa wanyama sisi wananchi ndiyo tumeenda kuwafata kule hata wao wanatushangaa kwamba kwanini sisi maeneo yetu wananchi wameyasogelea. Ndivyo sasa sisi kama Serikali tunajitahidi angalau kuwa tunawaondoa wale tembo kuwarudisha kwenye maeneo ya hifadhi. Lakini tutambue kwamba wananchi ndiyo tunaowafuata hawa tembo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, lengo la kutoza hiki kiwango ni kuzuia hawa wafugaji sasa kutoingiza mifugo yao kwenye hifadhi, na niombe Waheshimiwa kwenye hili tushirikiane lisionekane kama ni la Wizara ya Maliasili ya Utalii sheria hizi tumezitunga sisi wenyewe na utekelezaji wake basi tutekeleze sisi wenyewe. Wafugaji wanaaswa kutoingiza mifugo yao kwenye maeneo ya hifadhi ahsante.

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:- Je, ni kwa nini Serikali haitumii risiti za kielektroniki inapotoza faini za kuingiza mifugo kwenye Hifadhi zilizopo Sikonge?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. STEVEN L. KIRUSWA: Mheshimiwa Spika, ndiyo, ndiyo kabisa!

Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi na nitumie fursa hii kuiasa Wizara ya Maliasili na Utalii kwamba wanapofanya kila jitihada kuzuia mifugo isiingie ndani ya hifadhi hawafanyi juhudi kuzuia wanyama wasiingie ndani ya maeneo ya jamii.

Mheshimiwa Spika, kwa taarifa hiyo watambue pia kwamba mifugo na wanyamapori wote ni wanyama kuna maeneo ambayo wanaingiliana vizuri kiasi kwamba hata ningependekeza kwamba maeneo ambayo hamna wanyamapori kama misitu asili mifugo waruhusiwe kulisha kwasababu wanatengeneza mazingira ya ekolojia ya majani katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, swali langu ni kwamba kwa vile kuna hako kafuta jasho au kifuta machozi hawa wanyama wanapoingilia katika maeneo ya jamii.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba hicho kifuta machozi au kifuta jasho kinawahishwa kwasababu kuna tabia ya kuiweka mpaka hata mtu anakuja kupewa ameshasahau na maumivu aliyoyapata?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ni kweli wananchi wanapokutana na adha hii ya tembo kuingia kwenye mashamba yao Wizara ya Maliasili na Utalii ina utamaduni wa kulipa kifuta jasho, na kifuta jasho kinategemea ni aina gani ya uharibifu uliofanyika.

Mheshimiwa Spika, kuna waliopata adha ya kupoteza maisha, lakini kuna wale ambao wamepoteza mazao huwa tunafanya tathmini pale tu ambapo tembo wanakuwa wameingia kwenye maeneo hayo na baada ya kufanya tathmini basi Serikali huwa inachukua jukumu la kulipa kifuta jasho.

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka huu wa fedha tumetenga bilioni mbili kwa ajili ya kulipa kifuta jasho. Nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kifuta jasho cha aina yoyote ambacho kinatokana na uvamizi wa tembo Serikali itakilipa ahsante.