Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 17 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 146 2021-04-27

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA aliuliza:-

Je, ni kwa nini Serikali haitumii risiti za kielektroniki inapotoza faini za kuingiza mifugo kwenye Hifadhi zilizopo Sikonge?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph George Kakunda, Mbunge wa Sikonge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu ya Sheria ya Wanyamapori Na.5 ya Mwaka 2009, ni kosa kwa mtu yeyote akiwemo mfugaji kuingiza mifugo kwenye maeneo yaliyohifadhiwa. Serikali iliweka sheria hii sio kwa ajili ya kujipatia mapato bali kudhibiti uharibifu ikiwemo uvamizi, ujangili na uingizaji wa mifugo ndani ya maeneo hayo kwa lengo la kuyatunza.

Mheshimiwa Spika, katika jitihada za kudhibiti upotevu wa mapato, Serikali ilianzisha mfumo wa TEHAMA kwa ajili ya utoaji wa leseni au vibali, ukusanyaji wa takwimu na mapato ya vyanzo mbalimbali vya Sekta ya Maliasili na Utalii unaoitwa MNRT Portal ambao umefungamanishwa na Mfumo wa Government electronic Payment Gateway yaani GePG kwa ajili ya kutoa Control Number inayomwezesha mteja sasa yeyote yule kulipa. Aidha, baada ya kufanya malipo hayo mfumo wa MNRT Portal unatoa risiti ambazo zinatambulika na Mamlaka ya Mapato Tanzania yaani TRA.

Mheshimiwa Spika, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kuwa risiti zinazotolewa na mfumo huu ni halali kwa malipo ya Serikali sawa na zinazotolewa na mfumo wa Electronic Fiscal Devices yaani EFDs.

Mheshimiwa Spika, naomba kuwasilisha. (Makofi)