Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba Wananchi wa Jimbo la Ngara wananufaika na uchimbaji wa Madini ya Nickel unaotarajia kuanza katika eneo la Kabanga?

Supplementary Question 1

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Spika, ninashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa eneo hili la Kabanga Nickel kuna leseni nyingi zimechukuliwa hivi karibuni kuzunguka eneo hili. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba leseni hizi zilizochukuliwa hazitazuia uwekezaji wa msingi wa Tembo Nickel?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa vile kuna tathmini ilifanyika hapo awali kwa ajili ya kutoa fidia kwa wananchi wanaoishi kuzunguka mgodi huu na kwa vile tathmini hii ambayo ilishafanyika, ilifanyika kipindi kirefu na hivyo imeshapoteza uhalali; je, Serikali ina mpango gani wa kurudia kufanya tathmini ili wananchi wanaounguka Mgodi huu wa Kabanga ambao kwa sasa unaitwa Tembo Nickel waweze kupata fidia? Ahsante. (Makofi)

Name

Prof. Shukrani Elisha Manya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ndaisaba, Mbunge wa Jimbo la Ngara, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, uwepo wa leseni zinazozunguka mradi tarajiwa wa uchimbaji wa Tembo Nickel, ni kwamba mtu anapokuwa amepewa leseni ana eneo ambalo lipo katika coordinates na kwa maana hiyo anachimba katika eneo lake na uwepo wa leseni nyingine zozote zinazozunguka eneo la mradi hauna uhusiano wa kuzuia uchimbaji wa mtu aliye na leseni yake. Ni sawa na upangaji tu wa nyumba mtu ana kiwanja chake utaingia nyumbani kwako na mimi nitaingia nyumbani kwangu.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishe Mbunge kwamba kuwepo kwa leseni nyingine zozote zilizotolewa siku za karibuni hazitazuia kamwe uchimbaji unao tarajiwa wa mradi wa Nickel.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ni kuhusu tathmini; ni kweli kwamba tathmini ilishafanyika siku za nyuma na ikipita miezi sita mara nyingi tathmini hiyo kisheria inaonekana kwamba haifai na hivyo inabidi kurudiwa. Katika miradi yote ya uchimbaji mkubwa hakuna mradi ulioanza bila kufanya tathmini na wananchi kulipwa malipo stahiki. Siku zote tunawaelekeza watu hawa wanaofanya miradi mikubwa ya uchimbaji waweze kuwa na social license, kwamba waweze kuwa na mahusiano mazuri na jamii inayowazunguka.

Kwa hiyo tutawaelekeza Tembo Mineral Corporation kwamba warudie kufanya tathmini na walipe fidia ili hatimaye mradi uweze kuanza. (Makofi) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba Wananchi wa Jimbo la Ngara wananufaika na uchimbaji wa Madini ya Nickel unaotarajia kuanza katika eneo la Kabanga.