Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO K.n.y. MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itafanya zoezi la kuhakiki na kuweka alama kwenye mpaka wa Tanzania na Kenya kwa eneo la nchi kavu na baharini ili wananchi wa mpakani Wilayani Mkinga waondokane na kero ya muda mrefu ya kukamatwa na kutaifishiwa mali zao na askari wa Kenya?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. naomba niulize maswali mawilinya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Kijiji cha Jasini kwa Kata ya Moa na Mayomboni, Wilaya ya Mkinga wanapata usumbufu sana wa kukamatwa na askari wa Kenya na kwenda kushitakiwa Kenya na wakati mwingine mali zao kutaifishwa.

Je, ni lini sasa Serikali itahakikisha hali hii inakoma? Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili,...

SPIKA: Wanakamatwa kwa sababu gani?

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Spika, wanaonekana wameingia Kenya, wakivua Kenya, ni eneo la bahari.

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili, askari wa Kenya mara kadhaa wanaingia Jasini, hali ambayo ni hatari sana kwa nchi zetu hizi mbili.

Je, ni lini sasa Serikali itachukua hatua za haraka za kuhakikisha inaweka mipaka ili kuhakikisha Serikali ya Kenya na Tanzania zisije zikaingia kwenye migogoro? Asante nashukuru. (Makofi)

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA
MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza napenda nikiri ni kweli katika eneo la Jasini kwenye Kata ya Moa na Mayombo mara nyingi kumekuwa kukitokea ukamataji wa wananchi wa eneo hilo na hili pia liliwahi kutokea wakati pia tuko ziara kule, nilishafika mpaka Jasini.

Mheshimiwa Spika, lakini kinachotokea hapa ni kutokana na kwamba katika uimarishaji wa mpaka tumesema tunaimarisha kwanza maeneo ya nchi kavu kwa sababu majini katika kuweka maboya tayari mpaka nchi zote mbili ziridhie wapi maboya yawekwe, pamoja na kwamba, tunajua kuna ule mbali wa nautical miles 200 ambazo ziko kwetu, lakini hii haijaweza kufanyika kutokana na hali halisi ambayo kila ukitaka kuweka alama lazima mkubaliane wote.

Mheshimiwa Spika, lakini napenda kushukuru sana Balozi zetu, Ubalozi wetu wa Kenya pamoja na ule mdogo wa Mombasa. Nimshukuru sana Mheshimiwa Pindi Chana wakati yuko pale wametatua matatizo mengi kutokana na kesi hizi na sasa hivi balozi aliyeko pale, Consular Athumani Haji aliyeko Mombasa, ni juzi toka miezi sita iliyopita wameweza kutatua pia changamoto hiyo ya kuweza kukamatwa.

Mheshimiwa Spika, tatizo lililopo kutokuwekwa kwa maboya pale ni kutokana na makubaliano ya nchi mbili, lazima mkubaliane ndio muweke alama hizo. Bila kukubaliana hakuna nchi itakayoweza kuweka.

Mheshimiwa Spika, na kingine ambacho ni changamoto kule sasahivi wameanzisha sheria ya uvuvi ambayo chombo kinapoingia ziwani lazima ulipe dola 500 na ukikamatwa pale fine ni dola 300. Sasa mara nyingi wavuvi wetu wanakuwa hawana, lakini diplomasia imekuwa ikitumika wanajadiliana kati ya ubalozi n akule na watu wanatoka.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niseme tu kwamba katika swali lake la pili analosema ni lini hii itakomeshwa? Niwaombe tu muwe na Subira kwa sababu mchakato unaendelea katika suala zima la kuimarisha mipaka kama ambavyo nimesema katika jibu langu la msingi. Tukiimarisha mipaka hiyo ya nchi kavu ikikamilika suala la kuweka maboya ndilo limebaki kwa sababu tayari mpaka ulishabainishwa isipokuwa ni kuweka alama tu. Tutaweka mara tutakapokuwa tumekubaliana na wenzetu wa Kenya.