Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 15 Lands, Housing and Human Settlement Development Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 128 2021-04-22

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. MWANTUMU M. ZODO K.n.y. MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itafanya zoezi la kuhakiki na kuweka alama kwenye mpaka wa Tanzania na Kenya kwa eneo la nchi kavu na baharini ili wananchi wa mpakani Wilayani Mkinga waondokane na kero ya muda mrefu ya kukamatwa na kutaifishiwa mali zao na askari wa Kenya?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dunstan Luka Kitandula, Mbunge wa Mkinga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mpaka wa kimataifa kati ya Tanzania na Kenya una jumla ya urefu wa kilometa 817.71 ikiwa kilometa 758 ni nchi kavu na kilometa 59.71 ni ndani ya maji. Eneo la nchi kavu la mpaka huo linaanzia Ziwa Victoria, Wilaya ya Rorya Mkoani Mara hadi Jasini, Wilaya ya Mkinga Mkoa wa Tanga.

Mheshimiwa Spika, hadi sasa, sehemu ya mpaka wa Tanzania na Kenya yenye urefu wa kilometa 172 kutoka Ziwa Victoria hadi Ziwa Natron umeimarishwa na kuwekewa
alama 1,135. Kati ya alama hizo, alama 162 zimejengwa na kukarabatiwa na alama 973 zimejengwa kwa umbali wa mita 100 hadi 200 ili kuwezesha wananchi kuubaini mpaka kwa urahisi. Zoezi la kuimarisha mpaka kati ya Ziwa Natron hadi Namanga wenye urefu wa kilometa 128 kwa mwaka 2019/ 2020 liliahirishwa kutokana na kuzuka kwa ugonjwa wa Covid-19. Kutokana na uwepo wa ugonjwa huo, zoezi la kuimarisha mpaka uliobaki kati ya Tanzania na Kenya wenye urefu wa kilometa 586 kwa nchi kavu na kilometa 59.71 ndani ya maji limesimama hadi hapo nchi hizi mbili zitakapokubaliana. Urefu wa Mpaka katika Wilaya ya Mkinga katika mpaka huu ambao haujaimarishwa ni kilometa 52.96 ambayo ni nchi kavu.

Mheshimiwa Spika, sehemu ya mpaka ndani ya Bahari ya Hindi kutoka Jasini hadi kwenye alama ya utatu kati ya nchi ya Tanzania, Kenya na Ushelisheli ina mkataba wa makubaliano kati ya nchi hizi tatu… katikati ya Kenya na Tanzania ambao ulitiwa saini tarehe 23 Juni, 2009 Jijini Dar es Salaam isipokuwa alama zake za maboya hazijawekwa. Kazi ya kuweka maboya katika mpaka huu itafanyika baada ya kukamilika uimarishaji wa mpaka katika eneo la nchi kavu.