Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza:- Barabara ya kutoka Kibena (Stop Lupembe) mpaka Madeke C Mfiji, kilometa 125, imeshafanyiwa usanifu na upembuzi yakinifu tangu mwaka 2015. Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa barabara hii imekuwa ikipata ahadi nyingi sana za Serikali hasa kila wakati wa Uchaguzi mwaka 2015 imeahidiwa haikujengwa na leo inaahidiwa tena ndani ya Bunge lako Tukufu, wananchi wa Lupembe wanapenda kujua kuna utofauti gani wa ahadi za nyuma ambazo hazikutekelezwa na ahadi hii ya leo? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili Serikali ina mpango gani wa kuwalipa fidia wananchi ambao wataathirika na barabara hii hasa katika maeneo ya Nyombo, Kidegembye, Matembwe, Lupembe Barazani, Igombola, Mfiriga mpaka Madeke? Ahsante

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.
GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi za Serikali si za kubahatisha na namuomba nimuhakikishie kwamba ahadi ninayomwambia leo ni ahadi ya ukweli, awasiliane na uongozi wa TANROADS watamweleza wako kwenye taratibu za mwisho kabisa kutangaza hii barabara hizi kilomita 50 ili zianze kujengwa kwa kiwango cha lami na hasa tukitambua ni barabara ambayo inaunganisha mkoa wa Njombe na Mkoa wa Morogoro kupitia Mlimba Ifakara hadi Mikumi. Kwahiyo nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge.

Swali lake la pili ni kuhusu fidia ni kweli tathmini ilishafanyika watu walishatambuliwa na gharama za ulipaji wa fidia ulishahakikiwa nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba wananchi wote wa vijiji na kata alizozitaja watalipwa fidia yao kabla ya ujenzi kuanza. Hili litakwenda sambamba wakati ujenzi utakapokuwa unaanza wanafanya mobilization Serikali itakuwa inaendelea na kuwalipa ama kuwalipa fidia wananchi ambao watakuwa wameathirika na mradi huu ahsante.

Name

Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza:- Barabara ya kutoka Kibena (Stop Lupembe) mpaka Madeke C Mfiji, kilometa 125, imeshafanyiwa usanifu na upembuzi yakinifu tangu mwaka 2015. Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Naibu Spika, na mimi nakushukuru mvua hizi zinazonyesha nchi nzima zinanyesha nazo Dar es Salaam hali ya barabara za Dar es Salaam ni mbaya na nikisema ni mbaya uchumi wa Dar es Salaam ukianguka ni uchumi wa Taifa unaanguka mapato ya Dar es Salaam ndiyo yanasaidia kujenga nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara za Jimbo la Ilala leo Kariakoo haipitiki, Upanga haipitiki, Soko la Ilala halipitiki wananchi wanauza bidhaa zao sasa barabarani. Mwarobaini ni pamoja na mradi wa DMDP II kuweza kupitishwa haraka kusaidia wakazi wa Dar es Salaam na hasa Jimbo la Ilala.

Sasa naiomba Serikali lini sasa Serikali itaanza kutekeleza mradi huu ambao tayari umeshawasilishwa na TAMISEMI menu yote ya mahitaji ya barabara ipo tayari Hazina ni lini Serikali inatoa kauli kwa mradi huu unaanza lini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.
GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, katika majiji yetu tuna barabara za aina mbili ziko barabara ambazo ni kweli zinasimamiwa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi lakini tunasaidiana na Wizara ya TAMISEMI kwenye baadhi ya barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikiri kwamba kumekuwa na changamoto nyingi hasa kipindi cha mvua pale ambapo barabara zetu nyingi zinakuwa zimekatika lakini kama Mheshimiwa Zungu alivyosema Mbunge wa Ilala tayari upo mpango wa kuzitengeneza barabara hizi zikiwepo barabara zote za Majiji ya Dodoma Jiji la Mbeya, Jiji la Arusha na hata Jiji la Mwanza. Pengine rai yangu kubwa kwa wananchi ni kuhakikisha kwamba mengi ya matatizo tunayopata ni kwasababu aidha tumejenga kwenye mikondo ya maji kwa hiyo tunabadilisha mwelekeo wa maji. Lakini wakati fulani pia mifereji hii haisafishwi na kusababisha maji yanajaa na hivyo kutoka kwenye mikondo yake ya kawaida.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimuhakikishie Mheshimiwa Zungu tuna mpango kabambe kama Serikali wa kuhakikisha kwamba suala hili tunalifanyia mkakati wa kudumu ili tuweze kuachana na hii adha kati ya Wizara ya Ujenzi na Wizara ya TAMISEMI ahsante.