Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 13 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 112 2021-04-20

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza:-

Barabara ya kutoka Kibena (Stop Lupembe) mpaka Madeke C Mfiji, kilometa 125, imeshafanyiwa usanifu na upembuzi yakinifu tangu mwaka 2015.

Je, ni lini ujenzi wa barabara hiyo utaanza kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi napenda kujibu swali la Mheshimiwa Edwin Enosy Swalle, Mbunge wa Lupembe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, barabara ya Kibena - Lupembe – Taweta yenye urefu wa kilometa 125 ni Barabara ya Mkoa inayohudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Njombe. Kwa kutambua umuhimu wa barabara hii, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina pamoja na uandaaji wa nyaraka za zabuni kwa ajili ya taratibu za ununuzi wa Mkandarasi wa ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha huu wa 2020/2021, Serikali imetenga jumla ya Shilingi bilioni 5.96 kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa sehemu ya barabara ya Kibena – Lupembe yenye urefu wa kilometa 50. Aidha, wakati Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami kwa vipande vingine, Wizara yangu inaendelea kuihudumia barabara hiyo ili iweze kupitika majira yote ya mwaka. Ahsante.