Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ahadi ya ujenzi wa barabara ya Mtwara – Tandahimba – Newala – Masasi hadi Nachingwea kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kuulizwa maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa barabara hiyo sasa inaitwa kwa jina la dhihaka kwamba ni barabara ya kuombea kura na kwamba katika jibu la msingi Mheshimiwa Naibu Waziri amesema jumla ya Shilingi Bilioni 10 zimetengwa kwa bajeti ya mwaka 2020/2021 na sasa imebaki miezi miwili, naomba kuuliza swali, ni lini hasa ujenzi huo unaanza na kukamilika kwa kuwa hata Mkandarasi na ukusanyaji wa vifaa haujaanza? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kutokana na ubovu wa barabara hiyo vyombo vya usafiri vimekuwa vikitoza nauli kubwa. Umbali wa kutoza Sh.750 unatozwa Sh.3,000 na kuendelea. Je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Mtwara namna inavyoweza kukomesha ama kuwasaidia kumudu gharama za usafiri ili waweze kutatua changamoto mbalimbali ambazo zinawahitaji kusafiri? Ahsante. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA
M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Agnes Hokororo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Mbunge wa Viti Maalum wa Mkoa wa Mtwara kwa kuwasemea wananchi wake katika jambo muhimu sana la mawasiliano ya barabara. Kwenye swali lake la kwanza amesema ni kweli kwamba zimetengwa Shilingi Bilioni 10 na muda wa bajeti ya mwaka huu imeyoyoma sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge baada ya hapa tu baada ya maswali na majibu tutakaa naye kwa sababu hapa kuna mchakato fedha zipo zimetengwa kama kuna changamoto kama nilivyosema hakuna taarifa kule eneo la Mtwara hasa TANROADS tuwasiliane, tumpe majibu sahihi ili aweze kueleza wananchi wake ni lini barabara hii inaanza kutengenezwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili anasema nauli imepanda kwa sababu ya ubovu wa barabara kutoka 750 hadi 3,000 na nini kauli ya Serikali. Kauli ya Serikali ni kwamba, Serikali itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami kama ambavyo ilivyoahidi kwenye Ilani ya Chama Cha Mapinduzi. Naomba niwaambie wananchi wa Mtwara na maeneo ya jirani kwamba sasa barabara hii haitakuwa barabara ya kura itakuwa jambo halisi na litatekelezwa. Ahsante sana.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ahadi ya ujenzi wa barabara ya Mtwara – Tandahimba – Newala – Masasi hadi Nachingwea kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa barabara hii ya Mtwara inafanana kabisa na ahadi ya Serikali kupitia Ilani ya Uchaguzi katika barabara ya kujengwa kwa kiwango cha lami kuanzia Babati kupitia Sukuru – Olkasmenti - Simanjiro – Kibaya, Wilaya ya Kiteto. Je, Serikali ni lini itaanza ujenzi wa barabara hii ili kurahisisha huduma kwa wananchi wa Manyara? (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA
M. WAITARA): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Manyara, Mbunge wa Vijana, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme tu kwamba kazi inaendelea ilikwishaanza baadhi ya barabara tathmini imekamilika na ujenzi unaendelea. Zile barabara ambazo hazikufanyika mwaka wa fedha 2020/2021, zimewekewa mpango mkakati wa bajeti ijayo 2021/2022. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge wa Vijana, Mkoa wa Manyara, watu wa Manyara wasiwe na wasiwasi mpaka Simanjiro, tutatekeleza Ilani ya Uchaguzi kama ilivyoelekezwa na kama ambavyo ndio maagizo ya Viongozi wetu Wakuu hasa Mheshimiwa Rais Mama Samia Suluhu Hassan.