Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 13 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 111 2021-04-20

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha ahadi ya ujenzi wa barabara ya Mtwara – Tandahimba – Newala – Masasi hadi Nachingwea kwa kiwango cha lami?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Agnes Elias Hokororo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kupitia Wakala wa Barabara nchini TANROADS ilikamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa barabara ya Mtwara -Tandahimba – Newala - Masasi hadi Nachingwea yenye urefu wa kilometa 255 mwaka 2015. Mpango wa Serikali ni kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami kwa awamu kulinganana upatikanaji wa fedha. Hadi sasa Serikali imekamilisha awamu ya kwanza ya ujenzi huo katika sehemu ya Mtwara hadi Mnivata yenye urefu wa kilomita 50 kwa gharama ya Shilingi Bilioni 89.591.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa Serikali inaendelea na mipango ya kuanza ujenzi wa kiwango cha lami kwa sehemu iliyobaki ya Mnivata – Tandahimba – Newala - Masasi hadi Nachingwea kulingana na upatikanaji wa fedha. Aidha, katika mwaka wa fedha 2021 jumla ya Shilingi Bilioni 10 zilitengwa kwa ajili ya malipo ya mkandarasi wa barabara kwa sehemu ya kwanza ya Mtwara - Mnivata na kuanza maandalizi ya ujenzi wa kiwango cha lami kwa sehemu ya Mnivata - Tandahimba.

Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na juhudi za ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kupitia Wakala wa Barabara nchini imeendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali barabara hiyo ili kuhakikisha kuwa inapitika kwa majira yote. Pia napenda kumtaarifu Mheshimiwa Mbunge kuwa, baada ya Mheshimiwa Hayati Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu wa Tano kuiomba Benki ya Maendeleo ya Afrika kutukopesha fedha za ujenzi wa sehemu hii ya Mnivata – Tandahimba – Newala - Masasi yenye urefu wa kilometa 160, benki hiyo tayari imetembelea barabara hiyo na kuna dalili nzuri benki hiyo kugharamia ujenzi wa sehemu hiyo ya barabara. Ahsante.