Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kijiji cha Matandarani Kata ya Sitalike?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi tena niulize swali la nyongeza. Kwa kuwa Kijiji cha Matandarani hakina kabisa hata kisima kimoja na wananchi wanakunywa maji machafu siku zote; na kwa kuwa, mradi huu mpaka sasa hivi una asilimia 10 tu na mradi huu ni wa muda mrefu ambapo wananchi wanauona, lakini juhudi ambazo zinatakiwa zifanyike hazipo: Je, lini mradi huu utakwisha? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, vijiji vyote ambavyo amevitaja Mheshimiwa Naibu Waziri ni kweli havina maji kabisa: Mtisi hakuna maji kabisa, ukienda Kijiji kinachofuata cha Magula hawana maji kabisa; na huu mradi mmesema unaenda mpaka Ibindi, kata jirani, nako hakuna maji kabisa: Je, Serikali ina mkakati gani kupitia hii miradi na kuhakikisha inakwisha kwa haraka kwa sababu, wananchi wanapata taabu sana? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Awali ya yote napenda kumpongeza Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, amekuwa mfuatiliaji wa karibu sana katika suala hili la tatizo la maji katika maeneo haya ya Vijiji vya Matandarani, Ibindi, Mtisi na Magula.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kumwambia tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, kwa kupitia jitihada zake, mimi binafsi kama Naibu Waziri ninakuhakikishia mara baada ya hili Bunge tutakwenda pamoja mpaka kwenye mradi huu. Usanifu wa mradi huu unatuonesha utakamilika mwezi Septemba. Hata hivyo, tutajitahidi kwa hali na mali tufanye kazi hii usiku na mchana na kurejesha muda nyuma ili mradi huu sasa usiishe Septemba, basi tujitahidi hata ikiwezekana uishe kabla ya usanifu muda unavyoonekana. (Makofi)