Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 13 Water and Irrigation Wizara ya Maji 108 2021-04-20

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Kijiji cha Matandarani Kata ya Sitalike?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anna Richard Lupembe, Mbunge wa Jimbo la Nsimbo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatekeleza mradi wa maji wa Magula ambao unahusisha ulazaji wa mabomba ya usambazaji umbali wa kilomita 14.9, ujenzi wa tanki la ujazo wa lita 200,000 na nyumba ya mtambo wa kusukuma maji. Ujenzi wa mradi umeanza mwezi Machi, 2021 na unatarajiwa kukamilika mwezi Septemba, 2021 kwa gharama ya shilingi milioni 545.62. Mradi huo utanufaisha jumla ya vijiji vitatu ambavyo ni Mtisi (Magula), Matandarani na Ibindi.