Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya kilometa 200 kutoka Kilyamatundu kupitia Ilemba, Muze, Mfinga mpaka Majimoto?

Supplementary Question 1

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri yanayoleta matumaini makubwa kwa wananchi wa Jimbo la Kwela naomba nitoe alert kwa Serikali, mtaalam wa upembuzi yakinifu ambaye yupo site speed yake ni ndogo sana. Niombe tu close follow-up kuhakikisha anamaliza kazi hiyo ndani ya kipindi cha mkataba.

Mheshimiwa Spika, swali langu la nyongeza; kwa kuwa barabara ya kutoka Mji Mdogo wa Laela kupitia Mnokola, Mwimbi mpaka kuunganisha nchi jirani ya Zambia ni ahadi ya Mheshimiwa Rais alipokuja kwenye kampeni. Wananchi wa maeneo ya Kata hizo zilizopo pembezoni mwa barabara wamekubali kuachia reserve ya barabara ili ijengwe kwa kiwango cha lami kwa sababu ni muhimu kwa uchumi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga na Mkoa wa Rukwa kwa ujumla. Naomba kupata commitment ya Serikali ni lini barabara hii itafanyiwa upembuzi yakinifu ili baadaye iweze kujengwa kwa kiwango cha lami?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano alipofanya ziara Mkoa wa Rukwa aliahidi ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka katika Kijiji cha Kaengesa - Seminari ya Kaengesa - Kitete kilometa saba na tayari upembuzi yakinifu umekamilika. Ni lini barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami kwa kuwa wananchi wanaisubiria kwa hamu na wanataka sana kuipata hiyo barabaa ya lami? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Deus Sangu, Mbunge wa Kwela, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tumechukua ushauri wake na tutahakikisha kwamba TANROADS wanamsimamia mkandarasi ili aweze kukamilisha usanifu wa kina unaoendelea ndani ya mkataba.

Mheshimiwa Spika, maswali yake mawili ya barabara ya Lahela kwenda nchi jirani lakini pia Kaengesa kwenda Kitete kilometa saba, kama alivyosema hizi ni ahadi za viongozi wetu wa Kitaifa. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Jimbo la Kwela, tumesikia na huo ndio ukweli kwamba ahadi zote zilizoahidiwa na viongozi wetu wa kitaifa zitaendelea kama zilivyoahidiwa. Kwa hivyo, Mheshimiwa Mbunge aelewe kwamba tunapoanza upembuzi na usanifu tayari ni hatua ya utekelezaji wa ahadi hizo. Tukishakamilisha basi nimhakikishie kwamba barabara hizo zitajengwa kwa kiwango cha lami kulingana na upatikanaji wa fedha kama viongozi wetu wa kitaifa walivyoahidi. Ahsante.