Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatengeneza kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mbalizi – Mkwajuni ili kuepusha adha wanayokutana nayo Wananchi hususani kipindi cha mvua?

Supplementary Question 1

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kunipa nafasi. Pamoja na majibu ya Naibu Waziri, naomba kuuliza swali la nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, hali ya barabara ni mbaya sana kwa wananchi wa Wilaya ya Songwe na hali hii imesababisha wananchi kupoteza maisha, ikiwa ni pamoja na kuzikosa huduma za muhimu na za msingi ambazo wanatakiwa kuzipata katika Ofisi ya Mkoa. Je, Serikali haioni umuhimu wa kulichukulia jambo hili kwa dharura, ili wananchi waweze kuepukana na changamoto ambayo imekuwa ikiwakabili kila mwaka katika Wilaya ya Songwe? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara anayoisema mwaka huu ilikuwa imesimama kwasababu ya mvua nyingi ambayo inaendelea kunyesha. Na kuna daraja linalounganisha Kijiji cha Tanga na Mbala ambapo mto ulitoka kwenye njia yake ukakata barabara na ukawa umetengeneza bwawa.

Mheshimiwa Spika, tunavyoongea na hasa kupitia Mbunge Mulugo wa Jimbo la Songwe tumekuwa mara nyingi tunawasiliananae na anafahamu fika kwamba, hadi sasa wakandarasi wako site. wameanza Alhamisi ya wiki iliyopita, tumapata fedha shilingi milioni 700 kwa ajili ya kukarabati batabata hiyo na kurejesha mawasiliano.

Mheshimiwa Spika, lakini baada ya hiyo barabara kukatika kuna barabara nyingine ambayo walikuwa wanapitia sasa Chunya – Mbeya kwenda Songwe. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, suala hilo lipo na tayari wakandarasi wako site na milioni 700 ziko tayari kwa ajili ya kuendesha mawasiliano ya barabara. Ahsante.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatengeneza kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mbalizi – Mkwajuni ili kuepusha adha wanayokutana nayo Wananchi hususani kipindi cha mvua?

Supplementary Question 2

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona, kwa kuwa, changamoto ya barabara ya Mbalizi – Mkwajuni inafanana kabisa na changamoto ya barabara inayoanzia Sepuka – Ndago hadi Kizaga. Na barabara hii tumekuwa tukiiulizia mara kwa mara, lakini tunaambiwa ipo kwenye upembuzi yakinifu. Je, ni lini Serikali itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami, ili kuchochea maendeleo ya Wilaya ya Ikungi pamoja na Wilaya ya Iramba? Nakushukuru.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Aysharose Matembe ambaye kwa kweli mara nyingi amekuwa akifuatilia, si tu barabara hii ya Sepuka – Ndago hadi Kisanga, lakini amekuwa akifuatilia barabara nyingi za Mkoa wa Singida.

Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, hizi barabara ni kati ya zile barabara ambazo zimeainishwa kwenye Ilani yetu ya Uchaguzi kwa ajili ya kukamilisha upembuzi yakinifu, lakini pia na usanifu wa kina, ili iweze kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mbunge avute Subira tupitishe bajeti tuone kama hizi barabara zitakuwa ni kati ya ambazo tutaanzanazo kwa mwaka huu. Ahsante sana.