Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 12 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 99 2021-04-19

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itatengeneza kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka Mbalizi – Mkwajuni ili kuepusha adha wanayokutana nayo Wananchi hususani kipindi cha mvua?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Simon Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Mbalizi – Chang’ombe – Mkwajuni – Patamela – Makongolosi yenye urefu wa kilometa 117 ni barabara ya Mkoa inayounganisha Mkoa wa Mbeya na Songwe na inahudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Mbalizi hadi Galula yenye urefu wa kilometa 56.

Aidha, taratibu za ununuzi kwa ajili ya kumpata Mhandisi Mshauri wa kufanya kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina zizonaendelea kwa sehemu ya Galula – Mkwajuni - Makongolosi kilometa 61 zinaendelea. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi kwa kiwango cha lami kwa sehemu ya Mbalizi hadi Galula chenye urefu wa kilometa 56 ambayo upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umekamilika.

Mheshimiwa Spika, wakati ujenzi kwa kiwango cha lami ukisubiri upatikanaji wa fedha, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), inaendelea kuifanyia matengenezo ya aina mbalimbali kila mwaka barabara hii. Ahsante.