Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ali Hassan Omar King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Jang'ombe

Primary Question

MHE. ALI HASSAN OMAR KING aliuliza:- Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo la makazi kwa askari wa Jeshi la Polisi na Mheshimiwa Rais aligusia azma hiyo alipokuwa akilihutubia Bunge hili la Kumi na Moja kwenye kikao cha ufunguzi. Je, Serikali imepanga kujenga mikoa mingapi majengo hayo ikiwemo Zanzibar?

Supplementary Question 1

MHE. ALI HASSAN OMAR KING: Mheshimiwa Spika, ahsante.
Kwanza napenda kumshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri na Wizara hii ya Mambo ya Ndani kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kuimarisha ulinzi na usalama katika nchi yetu.
Mheshimiwa Waziri atakubaliana na mimi kwamba katika majengo hayo ambayo yamejengwa 360 kwa misimu hiyo iliyopita ni jengo moja ninalolikumbuka mimi ambalo lipo pale Mkoa wa Mjini - Ziwani Polisi kwenye Jimbo langu. Pia Serikali imejenga jengo lingine kwa upande wa Zanzibar kule Pemba, haya majengo ukitazama ki-percentage ni madogo zaidi. Lakini mimi sina uhakika na taarifa hizi za 360; sasa namuuliza Mheshimiwa Waziri katika 360 ni majengo mangapi yalijengwa kule Zanzibar na katika haya 4,130 mangapi yanatarajia yatajengwa kule Zanzibar? Hilo swali la kwanza.
Mheshimiwa Spika, swali la pili Seriklai iliji-commit katika mwaka 2011, Juni kwamba kwa kupitia bajeti wa mwaka ule ingelifanya ukarabati majengo ya Ziwani Polisi, lakini pia wangelijenga na uzio na mpaka hivi sasa ninavyozungumza kwamba askari wanajitegemea wenyewe kufanya ukarabati katika nyumba ambazo wanaishi.
Je, Waziri atanihakikishia ni lini Serikali itakuja kufanya ukarabati wa majengo yale ya Ziwani Polisi pamoja na kujenga uzio? Ahsante sana.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kwanza nichukue fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge wa Jang‟ombe kwa ushirikiano wake mzuri sana ambao anatupa kwani ameshiriki katika ujenzi wa Kituo cha Afya pale Ziwani pamoja na uchimbaji wa kisima cha maji. Tunampongeza sana na tunamuahidi ushirikiano zaidi.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na maswali yake mawili, ni kwamba mradi wa nyumba 4,136 ambazo tunatarajia tujenge ni nyumba 200 ambazo zinatarajiwa kujengwa Unguja na nyumba 150 zinatarajia kujengwa Pemba, kwa hiyo ukifanya jumla ya idadi ya nyumba zote 350. Pia ameuliza kuhusiana na zile nyumba ambazo zilijengwa kupitia mradi wa NSSF. Ni kwamba nyumba zilizojengwa ni kweli maghorofa yale yalikuwa ni mawili kwa maana ya Unguja na Pemba lakini yana uwezo wa kukaa familia 12 kila moja kwa hiyo kufanya jumla ya familia 24.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala la ukarabati wa nyumba za Ziwani ni kweli nyumba zile ni chakavu lakini kama ambavyo tunazungumza siku zote kwamba, nyumba hizi za Polisi nyingi ni chakavu. Ndiyo maana tuna mchakato wa kuweza kurekebisha nyumba hizi pamoja na kujenga mpya. Kwa hiyo, niseme tu kwamba tunafahamu gharama za ujenzi wa nyumba hizo, ukarabati huo ambao unakadiriwa kufika takribani shilingi milioni 400; kwa hiyo tutajitahidi kwamba pale fedha itakapopatikana tuweze kuanza hiyo kazi haraka itakapowezekana.
Mheshimiwa Spika, tunafahamu umuhimu wa nyumba za Ziwani, ikiwa ni Makao Makuu ya Jeshi la Polisi na chimbuko la historia hata Mapinduzi ya Zanzibar yalianzia pale.

Name

Raisa Abdalla Mussa

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALI HASSAN OMAR KING aliuliza:- Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo la makazi kwa askari wa Jeshi la Polisi na Mheshimiwa Rais aligusia azma hiyo alipokuwa akilihutubia Bunge hili la Kumi na Moja kwenye kikao cha ufunguzi. Je, Serikali imepanga kujenga mikoa mingapi majengo hayo ikiwemo Zanzibar?

Supplementary Question 2

MHE. RAISA ABDALLAH MUSSA: Mheshimiwa Spika, asante kwa kuniona kwa sababu ni mgeni ndiyo maana jina langu hukunitaja naitwa Raisa Abdallah Mussa, Viti Maalum kutoka Zanzibar CUF. Napenda nimuulize Mheshimiwa Waziri swali moja la nyongeza. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Waziri katika vituo vidogo vya polisi vilivyoko Zanzibar, kuna baadhi ya vituo vimehamwa na nikutajie kwamba kituo cha Kidongo Chekundu Mentally Hospital, pale ni kituo muhimu sana kwa maeneo yale ya Kidongo Chekundu na Sogea, sasa hivi kile kituo kimehamwa na pamekuwa hasa kama gofu mpaka pamefanywa vijana wamekaa maskani yao pale pembeni yake.
Mheshimiwa Naibu Waziri, nataka uniambie una mpango gani na kukihuisha kituo kile cha Polisi cha Kidongo Chekundu? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ni kweli kuna baadhi ya vituo vya polisi ambavyo kidogo havifanyi kazi ikiwemo kituo hicho ambacho nilizungumza Mheshimiwa Mbunge, lakini pia kuna kituo cha Vuga na Shaurimoyo.
Mheshimiwa Spika, lakini kuna sababu mbalimbali ambazo zinasababisha vituo hivi kwa muda visiweze kufanyakazi. Vingine ni kwamba mahitaji ya vituo katika maeneo hayo yanakosekana umuhimu kulingana na changamoto za uhalifu na ukaribu wa vituo vingine vikubwa vya polisi vilivyopo maeneo hayo. Hata hivyo, kutokana vilevile na uhaba wa idadi ya askari waliopo tunashindwa kufungua vituo vyote katika maeneo yote ya Zanzibar.
Mheshimiwa Spika, sasa niseme tu kwamba, kituo cha Kidongo Chekundu ni moja kati ya vituo hivyo, hata hivyo nimuhakikishie Mbunge pamoja na wananchi wanaosikiliza kwamba Serikali haijakitupa kituo hicho, pale ambapo mahitaji yatakapoonekana ya muhimu tutakifanyia ukarabati na kuweza kukitumia kwa haraka sana.