Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 16 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 136 2016-05-10

Name

Ali Hassan Omar King

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Jang'ombe

Primary Question

MHE. ALI HASSAN OMAR KING aliuliza:-
Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo la makazi kwa askari wa Jeshi la Polisi na Mheshimiwa Rais aligusia azma hiyo alipokuwa akilihutubia Bunge hili la Kumi na Moja kwenye kikao cha ufunguzi.
Je, Serikali imepanga kujenga mikoa mingapi majengo hayo ikiwemo Zanzibar?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ali Hassan King, Mbunge wa Jang‟ombe, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza kuchukua hatua za makusudi kukabiliana na uhaba wa nyumba za Jeshi la Polisi. Kwa kutumia mifuko ya Hifadhi ya Jamii, chini ya mpango wa mikopo wenye riba nafuu Serikali imeshajenga nyumba 360 katika Mikoa ya Dar es Salaam, Unguja na Pemba.
Mheshimiwa Spika, Serikali pia inakusudia kujenga nyumba nyingine 4,136 katika mikoa 17 ya Tanzania Bara na Zanzibar. Aidha, Serikali itaendelea kutatua changamoto za uhaba wa nyumba za askari kwa kutumia njia mbalimbali ikiwemo mikopo yenye riba nafuu, Miradi Shirikishi (PPP) na kwa kutumia fedha za bajeti ya Serikali kadri hali ya uchumi itakavyokuwa ikiimarika.
Mheshimiwa Spika, mkakati huu utakwenda sambamba na Mipango ya Maendeleo ya Serikali ukilenga kufikia idadi ya nyumba za makazi kwa askari wote waliopo sasa na watakaotarajiriwa kuajiriwa baadaye.