Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya Kusini Unguja?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba nimjibu maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Naibu Spika, je, katika bajeti ya mwaka huu wa fedha kumetengwa fedha kwa ajili ya ujenzi wa ofisi hiyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili. Je, Mheshimiwa Naibu Spika uko tayari kuambatana ili twende ukajionee katika eneo hilo mwenyewe kwa macho yako hali halisi ya kusaidia kuhamasisha wananchi wako wa Mkoa wa Kusini Unguja, ili na wao wajue kwamba, wewe Naibu wao unafanya kazi vizuri? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo nimeeleza kwenye jibu langu la msingi, kukwama kwa kituo hiki kulikuwa kunasababishwa na upungufu wa fedha ambao sasa unatokana na ufinyu wa bajeti. Je, naulizwa, katika bajeti hii tumeingiza hiyo?

Mheshimiwa Naibu Spika, nimwambie kwamba, katika bajeti hii haikuingizwa, lakini nimuahidi tu kwamba, katika bajeti ijayo tutajitahidi hii Ofisi ya OCD Wilaya ya Kusini Unguja na ofisi nyingine na maeneo mengine ambayo yana uhitaji wa vituo hivi tutajitahidi tuhakikishe kwamba, tunapeleka au tunaendeleza ujenzi. Hasa ule ujenzi ambao umekwama wa vituo vya polisi katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini swali jingine je, nipo tayari kuambatananaye mama yangu?

Mheshimiwa Naibu Spika, nikwambie. Kwa ridhaa kabisa niko tayari kuambata na Mheshimiwa Mbunge tuende huko tukaangalie hilo eneo. Na itakuwa vizuri kwa sababu, tukifika huko tutawakusanya wananchi…

MBUNGE FULANI: Sio wewe.

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: …lakini
pia tutakaa na wadau ili kuhakikisha kwamba, tunawashajihisha kujenga kituo hiki, ili wananchi wa maeneo hayo, hasa maeneo ya Makunduchi, Kizimkazi, Mtende, Bwejuu, Paje na Jambiani na maeneo ya karibu waweze kupata huduma za ulinzi na usalama kama wanavyopata wananchi wengine. Nakushukuru.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya Kusini Unguja?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipatia swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Kituo cha Polisi Kisaki ambacho kiko Morogoro Vijijini kwa umuhimu wake kina matatizo ya usafiri. Je, ni lini kitapewa usafiri angalau pikipiki?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nikiri kwamba, bado tuna changamoto ya usafiri hasa katika maeneo ya vituo vya polisi, ikiwemo pikipiki na gari na aina nyingine za usafiri. Sasa nimwambie tu Mheshimiwa kwamba, aendelee kuvuta subira, Serikali kama Serikali tumo mbioni kuhakikisha kwamba, vituo vya polisi na maeneo mengine ambayo yanatoa huduma za ulinzi na usalama kwa wananchi tunahakikisha tunapeleka hivyo vyombo vya usafiri, ili sasa wananchi waweze kupata hizo huduma kama inavyotakiwa. Nakushukuru.

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya Kusini Unguja?

Supplementary Question 3

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Suala la Mkoa wa Kusini Unguja ni sawasawa na suala la Mkoa wa Kaskazini Unguja. Je, ofisi iliyokuweko Mkokotoni itamalizika lini? Maana huu mwaka wa tano unakwenda wa sita, bado kumalizika?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ofisi ile ipo kwa muda mrefu na ujenzi wake ulikwama hapa katikati, lakini nimhakikishie tu kwamba, Mheshimiwa Mbunge ukarabati na kuendelea kumalizika ujenzi wa jengo lile sasa hivi umo mbioni. Na kama atakuwa ameanza kupita kwa muda huu anaweza akayaona mabadiliko ya ujenzi ule.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niwaombe wananchi, hasa wa Mkoa wa Kaskazini Unguja, jambo lao tayari lipo na linatekelezwa na muda si mrefu sana wataanza kutumia kituo kile na wataendelea kupata huduma za ulinzi na usalama katika maeneo yale, hasa ya Mkokotoni, maeneo ya Donge, maeneo ya Mkwajuni na maeneo mengine ya Mkoa wa Kaskazini Unguja. Ninakushukuru.

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya Kusini Unguja?

Supplementary Question 4

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana; na mimi kwa niaba ya wananchi wa Biharamuro ningependa niongezee swali la nyongeza. Wilaya ya Biharamuro ni miongoni mwa wilaya kongwe kabisa za nchi hii lakini ukiingia katika mazingira ya polisi wa Biharamuro wanapoishi, bado wanaishi kwenye nyumba zilizojengwa na Mkoloni pale. Lakini mazingira ya kazi ni magumu wote mnajua kumekuwa na majambazi kule lakini vijana wale wanajitahidi kupambana nao usiku na mchana na hali yetu ni shwari kabisa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa maswali niliyonayo ni mawili, ni lini tutajengewa kituo kipya cha Polisi, ikizingatiwa tayari hati iko pale na kiwanja kipo tayari? Lakini pili…

NAIBU SPIKA: Moja tu Mheshimiwa; moja tu.

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa ruhusa yako, nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, naendelea kukiri tena kwamba bado tuna changamoto hasa kwenye usafiri, makazi na Vituo vya Polisi. Kwa kuwa, kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge amesema, tayari wana hati ambayo inawamilikisha wao waweze kujengewa eneo zuri waweze kupata jengo zuri ambalo litatoa huduma za ulinzi na usalama kwa wananchi, nimwambie tu kwamba aendelee kustahimili na mimi nalichukua hili tunakwenda kulifanyia kazi ili tuhakikishe kwamba katika eneo lake wanapata kituo kikubwa kizuri na cha kisasa ambacho kitaendelea kutoa huduma kwa wananchi na wananchi wakaendelea ku-enjoy hiyo huduma ya ulinzi na usalama katika eneo hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru.

Name

Ravia Idarus Faina

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Makunduchi

Primary Question

MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya Kusini Unguja?

Supplementary Question 5

MHE. RAVIA IDARUS FAINA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Napenda kumuuliza Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Je, ni lini nyumba za Askari wa Wilaya ya Kusini zitafanyiwa marekebisho kwasababu hali yake ni mbaya sana? Inafikia hatua kwamba baada ya kupigiliwa misumari hizo nyumba zimewekewa vipande vya matofali na mawe; kwa katika kipindi hiki cha mvua ni hali ngumu sana za wale askari. Je lini nyumba hizo zitafanyiwa marekebisho? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nijibu swali la Mheshimiwa Ravia Idarus Faina Mbunge wa Jimbo la Makunduchi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, sikuwa na uhakika sana kama kuna nyumba zimewekwa mawe badala ya kuwekwa bati; lakini kubwa niseme kwamba hata katika bajeti ambayo tuliyonayo mwaka huu tayari ujenzi wa nyumba hizi umezungumzwa na hatua za ujenzi wa nyumba hizi upo mbioni. Na si nyumba hizi tu tayari tuna mpango wa kujenga kituo kikubwa cha Polisi katika Mkoa wa Kusini na nyumba za kukaa maaskari katika Mkoa wa Kusini. Kikubwa nimwambie Mheshimiwa Mbunge tuendelee kustahimili kidogo. Najua hili linamgusa na linamuuma kwasababu anawaona askari wanavyopata tabu.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini binafsi nafahamu hili kwasababu huo Mkoa ni wa kwangu. Niseme tu kwamba ninalichukua hili tunakwenda kulifanyia kazi na nyumba za kukaa askari polisi Wilaya ya Kusini hasa Makunduchi zitapatikana Inshallah.