Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 9 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 78 2021-04-14

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUM DAU HAJI aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Polisi wa Wilaya Kusini Unguja?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, sasa naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwantum Dau Haji, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Kusini Unguja:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa ofisi ya Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kusini Unguja ulianza mwaka 2008 na gharama ya ujenzi wa mradi ni shilingi 225,000,000/= mpaka kukamilika kwake. Mpaka sasa ujenzi huu uko kwenye hatua ya msingi na unagharamiwa na Serikali kupitia bajeti ya maendeleo, na ujenzi umekwama kwasababu ya kukosekana kwa fedha za kutekeleza mradi wa ujenzi kutokana na ufinyu wa bajeti.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Jeshi la Polisi imo katika kufanya jitihada mbalimbali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo wadau wa ulinzi na usalama pamoja na wananchi, ili kuchangia na kukamilisha mradi huo, ili uweze kuwasaidia wananchi na shughuli za ulinzi na usalama ziweze kupatikana katika eneo hilo la Wilaya ya Kusini, Mkoa wa Kusini Unguja. Ahsante sana.