Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza:- Je ni lini Serikali itaacha kuwatoza shilingi 600 wakati wa kuingia na kutoka Bandarini wananchi wa Visiwa vya Kasalazi, Yozu, Gembela na Soswa katika Jimbo la Buchosa kwa kisingizio cha uwekezaji?

Supplementary Question 1

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nina swali moja la nyongeza. Kwa kuwa suala hili limekuwa la muda mrefu sana, lina jumla ya miaka kama minne au mitano, wananchi wanaendelea kupata mateso ya kulipa 600 wakati wa kuingia na 600 wakati wa kutoka, wananchi hawa maskini. Mimi binafsi nimeshasumbuka sana suala hili nimezungumza na Mheshimiwa Kakoko, nimezungumza na Mheshimiwa Abood, nimezungumza na Mheshimiwa Waziri Mkuu. Bahati nzuri Mheshimiwa Waziri Mkuu amenijibu na barua ninayo hapa ya kwamba amewaagiza TPA washughulikie suala hili mara moja. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kutoa tamko hapa kwamba tozo hizo zitapunguzwa mara moja ili wananchi waweze kuondoka kwenye mateso? (Makofi)

Name

Eng. Dr. Leonard Madaraka Chamuriho

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shigongo, Mbunge wa Buchosa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama ilivyojibiwa katika swali la msingi tozo hizo zinatolewa kwa mujibu wa sheria na zinafuata tariff book ambayo ni ya TPA. kama ambavyo imejibiwa katika jibu la msingi, sasa hivi tunafanya majadiliano ili tuweze kupunguza tozo hizo kulingana na malalamiko ya wananchi ili tuweze kwenda kisheria. Hatuwezi kupunguza sasa hivi kwani ndiyo mambo haya haya ambayo yatazuka tena katika Ripoti ya CAG kwamba tumetoza kinyume na Tariff Book. Kwa hiyo, tunafanya marejeo hayo na tutakapoyakamilisha, tutawasiliana na vijiji vyote kama vilivyotajwa pale katika Visiwa vya Kasalazi, Yozu, Gembela watashirikishwa katika kikao cha wadau ili tuweze kupata tozo muafaka ambazo zitakubalika kwa wananchi wote. Ahsante. (Makofi)

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza:- Je ni lini Serikali itaacha kuwatoza shilingi 600 wakati wa kuingia na kutoka Bandarini wananchi wa Visiwa vya Kasalazi, Yozu, Gembela na Soswa katika Jimbo la Buchosa kwa kisingizio cha uwekezaji?

Supplementary Question 2

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Naishukuru sana Serikali ya Chama Cha Mapinduzi kwa kuunganisha wilaya na wilaya, mikoa na mikoa. Hata hivyo, ipo barabara inayoanzia Njuki – Ilongero – Kidarafa hadi Hydom. Barabara hii nimekuwa nikiiulizia mara kwa mara ambayo inaunganisha Mkoa wa Manyara na Mkoa wa Singida. Je, ni lini sasa Serikali itakamilisha barabara hii kwa kiwango cha lami ili kuongeza kasi ya ukuaji wa uchumi kwa Mikoa ya Manyara na Singida? Nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aysha Mattembe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa sasa tupo kwenye Mpango wa Bajeti ya Mwaka mpya wa Fedha. Naomba nimwahidi Mheshimiwa Mbunge baada ya Bunge hili Tukufu kipindi cha maswali tukae pamoja tuone utaratibu uliotumika. Kwa sababu, barabara zinaibuliwa kutoka ngazi ya Mkoa kuja ngazi ya Wizara, basi kama barabara hizo ambazo zina mahitaji muhimu sana katika maeneo uliyoyasema hazikuingizwa kwenye Mpango wa Bajeti mwaka huu tujipange kwa Mwaka wa Fedha ujao. Wananchi wa pale wavute subira, tupo tayari kufanya kazi ya kuhakikisha kwamba maisha yao na bidhaa zao zinapata nafasi na gharama nafuu kusafirisha ili kuweza kubadilisha maisha yao.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.