Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 8 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 65 2021-04-13

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza:-

Je ni lini Serikali itaacha kuwatoza shilingi 600 wakati wa kuingia na kutoka Bandarini wananchi wa Visiwa vya Kasalazi, Yozu, Gembela na Soswa katika Jimbo la Buchosa kwa kisingizio cha uwekezaji?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Eric James Shigongo, Mbunge wa Buchosa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kiwango cha tozo ya abiria wanaopita katika bandari ndogo zilizopo katika maeneo mbalimbali ya mwambao wa bahari na maziwa ni shilingi 600 kama ambavyo imeainishwa katika kitabu cha tozo cha Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA). Hata hivyo, TPA baada ya kupokea malalamiko ya wadau mbalimbali kuhusu tozo hizo, imeanza kuchukua hatua za kufanya marejeo ya tozo hizo kwa bandari zote ndogo nchini kwa kushirikisha wadau katika maeneo mbalimbali. Vikao vya wadau ikiwemo wananchi katika Visiwa vya Kasalazi, Yozu, Gembela na Soswa vitafanyika kwa lengo la kupokea maoni yao kabla ya kuidhinishwa kwa tozo mpya. Ahsante.