Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA K.n.y. MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya mabasi ya Mji wa Katesh?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nami nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Halmashauri ya Meru nayo ilikuwa victim ya withdraw ya mradi mkakati ambayo ilikuwa imetengenezwa mwaka ule wa 2019. Naomba kuuliza: Je, Serikali sasa iko tayari kuja kutekeleza ule mradi?

Mheshimiwa Spika, Mradi huo uko eneo la Tengeru mahali panaitwa Sadak, ulikuwa umeshatengenezwa na Serikali ilikuwa imeshachakata lile andiko na nilipofika kule Hazina nikakuta karibia pesa zinatoka, kuja hapa Bungeni nikaambiwa mradi umekuwa withdrawn: Je, ni hatua gani zinazoendelea kuhakikisha kwamba Halmashauri ya Meru nayo inawezeshwa, kwa sababu sasa hivi inashindwa kuhudumia wananchi kwani haina mapato ya kutosha?Ahsante sana.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ni kweli mwaka 2019/2020 Serikali ilijaribu kusitisha kwa muda miradi yote ile ambayo ilikuwa inasuasua. Sasa hivi nikuhakikishie kwamba, Serikali imejipanga na tumekubaliana tui-review; na miradi yote ile ambayo ilisitishwa, ile miradi ya kimkakati katika Halmashauri zote ambazo zilikuwa zimepangiwa awali, inakwenda kufanya kazi. Ahsante sana.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA K.n.y. MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya mabasi ya Mji wa Katesh?

Supplementary Question 2

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa, changamoto ya Hanang inafanana sana na changamoto iliyopo kwenye mji wetu wa Chemba. Ni bahati mbaya sana uwezo wa Halmashauri yetu, ni mdogo: sasa naomba kujua, ni lini Serikali itajenga stendi kwenye Mji wetu wa Chemba?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, nieleze tu kwa kifupi kwamba, ile miradi ya kimkakati katika Halmashauri ilikuwa na vigezo kwa kila Halmashauri kupata. Tuliainisha vigezo 13 ambavyo Halmashauri ikivikamilisha inapata ile miradi. Moja ya vigezo ikiwemo ni; katika miaka mitatu mfululizo, Halmashauri hiyo iwe imepata hati safi. Kwa hiyo, kama ulikuwa unakosa baadhi ya vigezo, basi ulikuwa hau-qualify kupata hiyo miradi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunaomba Waheshimiwa Wabunge kuhimiza Halmashauri zenu kutimiza vigezo vyote. Vigezo ambavyo vimekamilishwa, vinaletwa Ofisi ya Rais, TAMISEMI nasi tukiona kwamba Halmashauri ina-qualify, basi tunawa-guarantee kupata huo mradi kwa ajili ya kusaidia Halmashauri zetu kuongeza mapato yao ya ndani. Ahsante sana.