Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 8 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 62 2021-04-13

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA K.n.y. MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa stendi ya mabasi ya Mji wa Katesh?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Samweli Xaday Hhayuma Mbunge wa Hanang kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Hanang ni miongoni mwa mwa Halmashauri zilizokidhi vigezo vya kupatiwa fedha za ujenzi wa stendi ya mabasi kupitia Mpango wa Mradi Mkakati katika Halmashauri. Lengo la Serikali kuanzisha Mpango huu ni kuziwezesha Halmashauri kubuni miradi itakayoziongezea mapato ili kutoa huduma bora kwa wananchi.

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Stendi ya Mabasi ya Katesh wenye gharama ya shilingi bilioni 5.60 ni miongoni mwa miradi 20 ya kimkakati nchini ambayo utekelezaji wake ulisitishwa katika mwaka wa fedha 2019/2020 kutokana na changamoto mbalimbali zilizojitokeza kwenye hatua za mwanzo za utekelezaji. Serikali ilizifanyia kazi changamoto hizo kupitia timu ya wataalam iliyoundwa na kutafuta namna bora ya kutekeleza miradi hiyo.

Mheshimiwa Spika, timu ilitoa maoni kadhaa yaliyotakiwa kutekelezwa na Halmashauri ya Hanang ikiwa ni pamoja na kupitia upya vipengele vyote vya mkataba, hususan muda wa mkataba na masharti ya dhamana ya awali kwa maana ya advanced payment guarantee. Hadi Machi, 2021 Halmashauri ya Wilaya ya Hanang imekamilisha taratibu zote kama ilivyoelekezwa na timu ya wataalam tayari kwa kuziwasilisha Wizara ya Fedha na Mipango. Hivyo, mradi utaendelea baada ya Wizara ya Fedha kupitia nyaraka hizo na kujiridhisha.