Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kutumia maji ya Mto Ruvuma kwa ajili ya kujenga miradi mikubwa ya maji ambayo itatatua changamoto za maji katika Jimbo la Nanyamba na maeneo jirani?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza maswali ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, la kwanza; nafikiri mradi ambao Mheshimiwa Naibu Waziri ameujibu ni ule mradi unaotoa maji Mayembechini na kupeleka Manispaa ya Mtwara na Nanyamba itafaidika kwa kutoa maji Nanguruwe kupeleka Nanyamba: Serikali haioni sasa kwa sababu usanifu huu ni wa zamani, wafanye review ya usanifu ili maji yatoke moja kwa moja Mayembechini na kupeleka Nanyamba na hivyo kunufaisha Kata ya Kiromba, Kiyanga na Mbembaleo; na vile vile, itasaidia kupeleka Wilaya za jirani kama Tandahimba na Jimbo la Mtama jirani na Jimbo la Nanyamba? (Makofi)

Swali langu la pili; ili kuboresha upatikanaji wa maji katika Mji wa Nanyamba, pia mradi wa Makonde ambao unanufaisha Halmashauri nne lazima upatiwe fedha za kutosha za ukarabati: Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya ukarabati mkubwa wa Mradi wa Makonde ili Halmashauri ya Nanyamba, Tandahimba, Newala Mjini na Vijijini wapate maji ya kutosha? Ahsante sana.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa ukarabati wa mradi tunafahamu kuna baadhi ya maeneo miradi ipo chakavu ikiwepo Nanyamba. Tayari Wizara imeshatoa maelekezo kwa Wahandisi wetu walioko maeneo hayo na ukarabati huu unatarajia kuanza mapema iwezekanavyo.

Mheshimiwa Spika, kwa Mradi wa Makonde vile vile, tutaendelea kupeleka fedha kwa awamu kadiri tunavyopata ili kuhakikisha mradi huu wa Makonde kwa ukubwa wake na umuhimu wake, tutaendelea kuukarabati na kuuongezea thamani ili uendelee kutoa huduma kwa wananchi wa Nanyamba.

Mheshimiwa Spika, vile vile, napenda kumpongeza sana Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota kwa namna ambavyo ameendelea kufuatilia upatikanaji wa maji safi na salama ya kutosheleza katika Mji wa Nanyamba na tuseme tu kwamba kwa sisi Wizara tumejipanga kuhakikisha Nanyamba maji yanakwenda kupatikana. (Makofi)

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kutumia maji ya Mto Ruvuma kwa ajili ya kujenga miradi mikubwa ya maji ambayo itatatua changamoto za maji katika Jimbo la Nanyamba na maeneo jirani?

Supplementary Question 2

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Kwa kuwa suala la upatikanaji wa maji safi na salama bado ni tatizo sugu katika Mkoa wa Mtwara na hivyo kupelekea akina mama kutumia maji ya kuokota okota na hivyo kuongeza gharama za matibabu kwa sababu ya matazizo ya homa za matumbo na kadhalika.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba tunamaliza tatizo la kuongeza gharama za matibabu kwa sababu ya upatikanaji wa maji ya kuokota okota ambao unapelekea wananchi kuendelea kupata homa mbalimbali? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hokororo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya umuhimu wa upatikanaji wa maji katika Mkoa wa Mtwara, Serikali kwa kupitia Wizara ya Maji, tayari tumejipanga kuhakikisha tunakwenda kutumia maji ya Mto Ruvuma. Tutakapoweza kufanya mradi huu, adha ya maji katika Mji wa Mtwara, Nanyamba na maeneo yote ya mwambao ule yanakwenda kukoma kwa sababu itakuwa ni suluhisho la kudumu. Kwa hiyo, tunatarajia mwaka ujao wa fedha kutumia maji ya Mto Ruvuma.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kutumia maji ya Mto Ruvuma kwa ajili ya kujenga miradi mikubwa ya maji ambayo itatatua changamoto za maji katika Jimbo la Nanyamba na maeneo jirani?

Supplementary Question 3

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Nimekuwa nikisimama hapa mbele ya Bunge lako Tukufu kuulizia Mradi wa Maji Kitinku-Lusilile ambao umechukua muda mrefu sana kukamilika, lakini bila ya mafanikio yoyote. Ningependa kupata commitment ya Serikali, ni lini Mradi wa Maji Kitinku-Lusilile utakamilika? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote kwanza nimpongeze Naibu wangu kwa namna anavyojibu maswali vizuri. Hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kubwa nimefanya ziara katika Mradi ule wa Kitinku–Lusilile, moja ya changamoto kubwa ilikuwa juu ya deni la mkandarasi, alikuwa akidai kama milioni 700. Wizara tumekwishamlipa milioni 700 zile mkandarasi yule. Mkakati wetu ni kuhakikisha mradi ule unakamilika kwa wakati na wananchi wale wanapata huduma ya maji safi, salama na yenye kutosheleza. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kutumia maji ya Mto Ruvuma kwa ajili ya kujenga miradi mikubwa ya maji ambayo itatatua changamoto za maji katika Jimbo la Nanyamba na maeneo jirani?

Supplementary Question 4

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Wewe utakuwa shahidi hiki ni kipindi changu cha tatu katika Bunge lako Tukufu na siku zote tatizo kubwa kwenye Wizara ya Maji imekuwa ni vitu viwili, mosi; miradi kutokukamilika kwa wakati au ikikamilika haitoi maji. Hii WIzara tangu 2016 imekuwa ikitengewa pesa nyingi, lakini ufanisi na ubora na kile kinachokusudiwa, wananchi wapate maji safi na salama hakipo. Swali langu, je, Serikali ipo tayari kufanya ukaguzi maalum nini chanzo cha miradi kukamilika lakini maji hayatoki au ni nini kinachosababisha miradi ichukue muda mrefu? Ahsante. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nikushukuru. Nikiri, moja ya changamoto kubwa sana ya miradi yetu ya maji ilikuwa moja, usimamizi lakini Bunge lako Tukufu limeona hili na ndiyo maana tukaanzisha Wakala wa Maji Vijijini kwa maana ya RUWASA, lakini kuhakikisha wahandisi wote wa maji waliokuwa chini ya halmashauri kuja chini ya Wizara yetu ya Maji. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tumeshaainisha miradi zaidi ya 177 na RUWASA imeshaanza kuitatua miradi hiyo zaidi ya 85. Kubwa ambalo nataka niwaelekeze Wahandisi wa Maji pamoja na Wakandarasi, vipo vya kuchezea. Ukishiba, chezea kidevu chako au kitambi, si miradi ya maji, tutashughulikiana ipasavyo! Ahsante sana. (Makofi/Kicheko)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaanza kutumia maji ya Mto Ruvuma kwa ajili ya kujenga miradi mikubwa ya maji ambayo itatatua changamoto za maji katika Jimbo la Nanyamba na maeneo jirani?

Supplementary Question 5

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kidogo Wagogo mnapata shida kuita jina Hussein, jina langu ni Hussein Nassor Amar, ni Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale.

Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza nianze kuishukuru Serikali kwa kuendelea kukamilisha mradi ya maji katika Jimbo la Nyang’hwale. Mheshimiwa Naibu Waziri alikuja na tukafanya nae ziara. Tukawa na upungufu wa shilingi milioni 250 tu ili tuweze kukamilisha mradi huo. Je, Naibu Waziri, ahadi yake ataikamilisha lini ya kupeleka milioni 250 ili kuweza kukamilisha Mradi huo wa Nyang’hwale? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hussein Nassor wa Jimbo la Nyng’hwale, kama ifuatavyo;

Mheshimiwa Spika, hizi fedha tayari tuko kwenye utaratibu wa kuzipeleka, tutazipeleka katika awamu mbili, wiki ijayo tutajitahidi kupunguza awamu ya kwanza na baada ya hapo tutajitahidi kukamilisha kabla ya mwaka huu wa fedha kuisha.