Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 7 Water and Irrigation Wizara ya Maji 58 2021-04-12

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaanza kutumia maji ya Mto Ruvuma kwa ajili ya kujenga miradi mikubwa ya maji ambayo itatatua changamoto za maji katika Jimbo la Nanyamba na maeneo jirani?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Dadi Chikota, Mbunge wa Jimbo la Nanyamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Maji kutoka Mto Ruvuma ni miongoni mwa miradi mikubwa ya kimkakati ambapo Serikali inatarajia kuanza utekelezaji wake katika mwaka wa fedha 2021/2022 kulingana na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, aidha, kupitia RUWASA ukarabati na upanuzi wa Mradi wa Maji kwenye Vijiji vya Makongo na Migombani umekamilika na unatoa huduma kwa wananchi. Vilevile, visima viwili vimechimbwa, nyumba ya mtambo wa kusukuma maji, ulazaji wa bomba kuu kilomita 3.5, ujenzi wa tenki moja la ujazo wa lita 100,000 na ujenzi wa matanki mengine manne unaendelea kwa ajili ya kuboresha huduma ya maji Nanyamba Mjini. Pia utekelezaji wa miradi katika Vijiji vya Ngonja – Chawi, Mayembejuu, Nyundo A na B, Nitekela na Misufini upo katika hatua mbalimbali za utekelezaji.