Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya Chuo Kikuu cha Afya Mbeya pamoja na Ndaki ya Afya na Sayansi Shirikishi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam – Mbeya?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza na nishukuru kwa jibu kutoka kwa Wizara ya Elimu. Kutokana na umuhimu wa huduma ya afya na hasa kwa suala zima la kupatikana kwa wahudumu pamoja na madaktari katika kipindi hiki ambacho milipuko ya magonjwa imepamba moto. Je, Serikali haioni umuhimu wa kutumia ardhi ya Taasisi za Serikali zilizopo katika Wilaya ya Mbeya ikiwemo ardhi ya Tanganyika Packers ili iweze kukidhi mahitaji ya chuo hiki?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, hii Ndaki ya Afya ina mkakati au mpango gani wa ziada zaidi ya kufundishia ili tuweze kupata huduma nyingi kutokana na hili eneo kubwa ambalo watakuwa wamepatiwa sasa hivi na Serikali? Nashukuru sana.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli anayozungumza Mheshimiwa Mbunge kwamba tuna mkakati wa kupata eneo hilo amelizungumza linalomilikiwa na Tanganyika Packers, ambalo liko chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Wizara yangu ikishirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi lakini vilevile Wizara ya Ardhi pamoja na Menejimenti ya Chuo na Uongozi wa Wilaya tutahakikisha tunakwenda kupata umiliki wa eneo hilo ili kuweza kufanya ujenzi wa chuo hiki.

Mheshimiwa Spika, pindi tutakapopata eneo hili, basi Serikali inaweza kutenga bajeti sasa kuhakikisha kwamba tunakwenda kujenga hospitali kubwa ambayo pamoja na Ndaki hii inaweza kuambatanishwa na Ndaki nyingine ili kuweza kupata wataalam wengi zaidi kwa ajili ya kuhudumia Watanzania.

Mheshimiwa Spika, lakini sambamba na hilo, mkakati wa muda mrefu kama nilivyozungumza mwanzo ni kwamba Serikali inatambua jambo hilo na tutakwenda kushughulikia kwa kadri bajeti itakavyoruhusu. Ahsante.