Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 7 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 54 2021-04-12

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha miundombinu ya Chuo Kikuu cha Afya Mbeya pamoja na Ndaki ya Afya na Sayansi Shirikishi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam – Mbeya?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Oran Manase Njeza, Mbunge wa Mbeya Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Ndaki ya Afya ya Sayansi Shirikishi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ilihamia Mbeya mwezi Desemba, 2017 ili kupata hospitali kubwa ya kufundishia. Ndaki ilipewa nafasi katika majengo ya Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Mbeya, baadhi ya majengo yaliendelea kutumika kama yalivyokuwa na baadhi yalihitaji ukarabati.

Mheshimiwa Spika, Serikali kwa kupitia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, imefanya upanuzi na ukarabati mkubwa wa bwalo la chakula na ukarabati wa madarasa na maabara. Pia Chuo kilinunua na kufunga jenereta la dharura kwenye maabara. Kutokana na ufinyu wa nafasi ndani ya Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, kama mkakati wa muda mfupi, majengo matatu ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam yaliyopo eneo la Uzunguni yamekarabatiwa na kuwekewa samani ili yaweze kutumika. Pia Serikali imefunga vifaa vya TEHAMA katika majengo mbalimbali ya Chuo na kuweka mtandao wa internet kwa ajili ya kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia.

Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali wa muda mrefu ni kupata ardhi Jijini Mbeya ili kuanza ujenzi wa majengo ya Ndaki ya Afya na Sayansi Shirikishi. Mkakati huo utatoa fursa ya kuongeza miundombinu ya kisasa ya kufundishia na kujifunzia na kuongeza udahili wa wanafunzi wa shahada mbalimbali za Afya na Sayansi Shirikishi. Maombi ya ardhi yameshawasilishwa na ufuatiliaji unaendelea. Ahsante.