Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ali Juma Mohamed

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. ALI JUMA MOHAMED Aliuliza:- Je, Serikali kupitia Balozi zetu ina mkakati gani wa kusimamia mikataba ya vijana wanaokwenda kufanya kazi nje ya nchi?

Supplementary Question 1

MHE. ALI JUMA MOHAMED: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ambayo ameyatoa Mheshimiwa Naibu Waziri nilikuwa na swali moja tu la nyongeza.

Serikali ina mpango gani wa kutafuta fursa mbalimbali za ajira ambazo ziko katika nchi mbalimbali duniani, kwa ajili ya Watanzania hususan nchi ya Qatar ambayo mwakani ni wenyeji wa Kombe la Dunia? (Makofi)

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Ali Juma Mohamed, Mbunge wa Shaurimoyo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kuchangamkia fursa kwa ajili ya Watanzania kwenda kufanya kazi nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, pili, napenda kukufahamisha kuwa Serikali imeanza mazungumzo na nchi mbalimbali ambazo zina fursa ya ajira hizo, hasa zikiwemo nchi za Ghuba, ili kuwa na utaratibu maalum wa kutoa quarter maalum kwa ajili ya Tanzania. Ninapenda kutoa taarifa pia kwamba tayari Tanzania imesaini mkataba na nchi ya Qatar kwa ajili ya kuwa na quarter maalum ya watanzania kwenda kufanya kazi huko, hasa katika kipindi hiki ambako tunaelekea kwenye mashindano ya World Cup ambayo yanaanza Novemba mwakani 2022. Ahsante sana. (Makofi)