Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 5 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 65 2021-09-06

Name

Ali Juma Mohamed

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. ALI JUMA MOHAMED Aliuliza:-

Je, Serikali kupitia Balozi zetu ina mkakati gani wa kusimamia mikataba ya vijana wanaokwenda kufanya kazi nje ya nchi?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ali Juma Mohamed, Mbunge wa Shaurimoyo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni wajibu wa Serikali kuhakikisha Watanzania wanaopata fursa za ajira nje ya mipaka ya Tanzania wanafanya kazi katika mazingira mazuri na yanayolinda staha na utu wao. Katika kufanikisha azma hiyo Serikali imeweka utaratibu mzuri wa kutoa vibali vya ajira nje kupitia mamlaka zinazoshughulikia masuala ya ajira, ikiwemo Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TAESA) na Kamisheni ya Kazi Zanzibar kwa kushirikiana na Balozi za Tanzania nje.

Mheshimiwa Spika, utaratibu huo pamoja na mambo mengine unaelekeza kila mfanyakazi kuwa na wakala rasmi wa ajira, ambaye anatambuliwa na mamlaka tajwa ambao ndio waandaaji wa mikataba ya ajira nje inayopaswa kukidhi Sheria za Ajira za Tanzania na nchi anayokwenda kufanya kazi. Aidha, kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na Serikali mikataba hiyo pia inapaswa kuandaliwa kwa lugha inayoeleweka na vijana hao, ikiwemo Kiswahili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pamoja na Serikali kuweka utaratibu huo bado kumekuwa na changamoto zinazotokana na baadhi ya vijana wanaopata ajira nje kutozingatia utaratibu uliopo. Pia, baadhi ya vijana hao hawajitambulishi kwenye Ofisi za Balozi za Tanzania pindi wanapofika kwenye ajira zao Ughaibuni. Kutokana na hali hiyo Serikali kupitia Balozi zake imeweka mikakati ifuatayo:-

(i) kutambua Kampuni za Uwakala wa Ajira za Nje na kuzitaka ziwe na uhusiano wa kimkataba na Kampuni za Uwakala za Tanzania.

(ii) Kuendelea kutoa elimu kwa vijana wanaopata ajira nje kutoa taarifa zao na kuwasilisha nakala za mikataba yao ya ajira Balozini ili ziweze kuhakikiwa.

(iii) Serikali imeanza mchakato wa kuingia mikataba ya ajira na baadhi ya nchi ili kurasimisha upatikanaji wa ajira katika nchi hizo.

Mheshimiwa Spika, napenda kutoa rai kwa Watanzania ambao wana nia ya kufanya kazi nje ya mipaka ya Tanzania, kufuata utaratibu uliowekwa na mamlaka husika. Kwa kuwa pamoja na mambo mengine inawapa kinga na kuepuka mazingira mabaya ya kazi ambayo hayatarajiwi na pia kurahisisha kupata msaada pale unapohitajika. Ahsante sana. (Makofi)