Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kiasi cha shilingi milioni 200 zilizoahidiwa na Waziri wa Maji Mwaka 2017 alipotembelea mradi wa Jumuiya ya Watumiaji Maji wa Magubike Kata ya Nzihi uliokarabatiwa na WARID kwa kiasi cha shilingi bilioni 1.3?

Supplementary Question 1

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Maswali yangu ya nyongeza ni kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Spika, kule Magunga ukitoka Magunga kwenda Lumuli kuna mradi ambao ulihasisiwa na Marehemu Dkt. William Mgimwa zaidi ya miaka saba iliyopita bahati mbaya haukutekelezwa, lakini sasa tunaishukuru Serikali imepeleka kiasi cha milioni kama 200 hivi kuanza kwa kutengeneza tenki kwa kutumia force account, lakini ninaona kwamba kasi yake ni ndogo.

Je, Wizara ina mpango gani hata kwa kutumia Wakandarasi ili maji yale yafike Kata ya Lumuli ambapo wananchi wake wamesubiria kwa muda mrefu sana.(Makofi)

Swali la pili, kumekuwa na mradi ambao pia ulianzishwa na aliyekuwa Mbunge na Katibu wa Bunge hili George Francis Mlawa wa Nyamlenge. Mradi huu ulikuwa wa maji tiririka ambao ungezifikia Kata kama tano, ukianzia Lyamgugo, Luhota, Mgama, Bagulilwa mpaka Ifunda, lakini sasa mmebadilisha scope mnachimba visima, wasiwasi wangu ni kwamba ikitokea tetemeko la ardhi na kule tupo kwenye bonde la ufa, visima vile mkondo huwa unahama maji yanakosekana.

Je, Serikali sasa ina mpango gani kupeleka pesa za kutosha ili turudi kwenye scope ya zamani na maji yapatikane katika Kata hizo tano ambazo nimezitaja?

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kiswaga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru Mheshimiwa Kiswaga kwa kuishukuru Serikali ya Mama Samia, tayari Magunga kazi zinaendela pale tumeanza na hii milioni 200 lakini fedha tutaendelea kuleta kwenye migao inayofuata, lengo ni kuona wananchi wote wa eneo lile wanaendelea kupata maji ya uhakika ya kiwa safi na salama bombani.

Mheshimiwa Spika, kijiji cha Lumuli hapa kipo kwenye mpango wa fedha za mwaka 2021/2022 na mradi huu kadri ambavyo tumeweza kufanya mashirikiano na Mheshimiwa Mbunge tutautekeleza kwa kupitia Mkandarasi lengo iweze kufanyika kwa haraka na wananchi wa Lumuli nao waweze kunufaika na fedha hizi ambazo Mheshimiwa Rais ameendelea kutupatia Wizara ya Maji.

Mheshimiwa Spika, eneo la Nyamulenge pia lipo kwenye mpango wetu wa muda mrefu. Kwa sasa hivi tumechimba visima virefu ambavyo vinatumia pump za umeme kwa sababu ya kuona kwamba kwa muda huu wananchi waweze kuendelea kupata huduma ya maji. Lakini katika mipango ya muda mrefu kama ambavyo tumeendelea kuwasiliana mara kwa mara na tulishaweza kushauriana kwa muda mrefu katika mpango wa muda mrefu chanzo hiki cha Nyamlenge tutakuja kukitumia kwa mradi wa maji ya uhakika maji ya mserereko ambayo eneo lile litapata maji ya kutosha na vijiji vyote vinavyopitiwa na mradi huu vitaweza kunifaika.

Name

Neema William Mgaya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA Aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kiasi cha shilingi milioni 200 zilizoahidiwa na Waziri wa Maji Mwaka 2017 alipotembelea mradi wa Jumuiya ya Watumiaji Maji wa Magubike Kata ya Nzihi uliokarabatiwa na WARID kwa kiasi cha shilingi bilioni 1.3?

Supplementary Question 2

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, ndani ya Mkoa wa Njombe Wilaya ya Wanging’ombe kuna mradi wa maji wa Igando - Kijombe wenye thamani ya bilioni 12. Lakini mpaka sasa hivi tunavyozungumza ni bilioni mbili tu ambazo zimekwenda kwenye mradi ule na mkandarasi yuko site lakini amesimamisha mradi hule hauendelei kwa sababu Serikali haijapeleka pesa.

Je, lini Serikali itapeleka hizo bilioni 10 ili mradi ule uweze kukamilika na Wananchi wa Wilaya ya Wanging’ombe waweze kupata maji safi na salama? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la
Mheshimiwa Neema Mgaya, kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Spika, hili suala tumeshalifanyia kazi kama Wizara na kwa ushirikiano mkubwa ambao tumekuwa nae Mheshimiwa Neema pamoja na Mheshimiwa Dkt. Dugange, tumeweza kufatilia na fedha tutaleta mgao ujao tutaendelea kutoa fedha kidogo kidogo, tutaleta bilioni Moja ili kazi ziendelee na mgao unaofuata pia tutaendelea kuleta fedha kadri tunavyopata.