Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 62 2021-09-06

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. JACKSON G. KISWAGA Aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kiasi cha shilingi milioni 200 zilizoahidiwa na Waziri wa Maji Mwaka 2017 alipotembelea mradi wa Jumuiya ya Watumiaji Maji wa Magubike Kata ya Nzihi uliokarabatiwa na WARID kwa kiasi cha shilingi bilioni 1.3?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jackson Gedion Kiswaga Mbunge wa Kalenga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mradi wa maji Kijiji cha Magubike upo Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Mradi huo unahudumia vijiji sita vya Kata ya Nzihi ambavyo ni Nzihi, Kipera, Kidamali, Nyamihuu, Magubike na Ilalasimba. Kwa lengo la kuboresha huduma ya maji katika vijiji hivyo na kufikisha huduma ya maji katika vitongoji vingine ambavyo havina huduma ya maji, mwaka 2017 Waziri wa Maji aliahidi kutuma shilingi milioni 200 kwa ajili ya upanuzi wa mradi wa Magubike.

Mheshimiwa Spika, katika kutekeleza ahadi hiyo, Serikali mwezi Juni na Agosti, 2021 imetuma jumla ya shilingi milioni 180 ambapo kazi zilizofanyika ni pamoja na ujenzi wa tenki lenye ujazo wa lita tisini elfu katika kijiji cha Nzihi, ulazaji wa bomba umbali wa kilomita 11.25 kwa ajili ya jamii kuingiza maji majumbani. Ujenzi huo unatarajiwa kuanza mwezi Oktoba, 2021 na kukamilika ifikapo mwezi Januari 2022. Kukamilika kwa kazi hizo kutaboresha huduma ya maji katika vijiji husika pamoja na vitongoji vya Mji mwema B, Mbega na Kayungwa ambavyo havina huduma ya uhakika ya maji.