Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE K.n.y. MHE. HASSAN Z. KUNGU Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Umeme Wilayani Tunduru chenye uwezo wa kupokea 132 KV ambazo ni uhitaji halisi kwa Wilaya ya Tunduru, Nanyumbu na Masasi?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Moja ya changamoto inayosababisha Tunduru kukatika umeme mara kwa mara ni ubovu wa miundombinu ya kutoka Namtumbo kuja Tunduru na kutoka Tunduru kwenda Nanyumbu mpaka Masasi.

Je, Serikali haioni sasa ni muhimu kuweka nguzo za zege kutoka Namtumbo mpaka Tunduru na kutoka Tunduru mpaka Masasi ili kudhibiti uharibifu wa nguzo za umeme unaotokea mara kwa mara na kufanya umeme kukatika katika maeneo hayo? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Daimu na muuliza swali mwenyewe Mheshimiwa Hassan, kwa nia ya kuendelea kuhakikisha kwamba miundombinu inaendelea kuboreshwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli Mkoa wa Ruvuma kwa mwaka huu wa fedha umetengewa shilingi 1,200,000,000 kwa ajili ya marekebisho ya miundombinu mbalimbali ya umeme ikiwemo nguzo, transfoma na waya. Lakini kabla sijasema kuhusiana na uwepo wa nguzo za zege kwanza niwaombe Waheshimiwa Wabunge wote watusaidie katika kuhakikisha miundombinu yetu ya umeme inalindwa kwenye maeneo yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, huko huko Tunduru jana kuamkia leo na upo Mwenge, lakini wananchi wamechoma miundombinu ya umeme na kusababisha umeme kukatika katika maeneo hayo. Na ni kweli kwamba tunatoka kwenye nguzo za miti kwenda kwenye nguzo za zege kwenye maeneo yenye matatizo korofi. Maeneo ambayo kuna wadudu waharibifu kama mchwa, maeneo ambayo ni oevu yana majimaji, lakini pia kwenye maeneo ambayo ni ya kwenye hifadhi ambako hakuwezi kufikika mara kwa mara na wanyama waharibifu wanakuwa wanaiharibu ile miti yetu ya kushikilia umeme.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kwenye maeneo ambayo hayana matatizo hayo tunawaomba Waheshimiwa Wabunge, waendelee kuwa mstari wa mbele kuhamasisha ulinzi wa miundombinu yetu ili isiharibiwe.

Kwa hiyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Daimu kwamba maeneo ambayo nimeyataja yanayohitaji nguzo za zege yatapelekewa nguzo za zege na tayari tumeshaanza. Wazabuni wanaotengeneza nguzo za zege tumeshawapata na kwenye baadhi ya maeneo kama mnavyoona Waheshimiwa Wabunge, tayari tumeshazipeleka na tutahakikisha miundombinu inaboreshwa zaidi. (Makofi)