Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 4 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 52 2021-09-03

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE K.n.y. MHE. HASSAN Z. KUNGU Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Umeme Wilayani Tunduru chenye uwezo wa kupokea 132 KV ambazo ni uhitaji halisi kwa Wilaya ya Tunduru, Nanyumbu na Masasi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Zidadu Kungu, Mbunge wa Tunduru Kaskazini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Shirika la Umeme nchini (TANESCO) inaendelea na upembuzi yakinifu kwa ajili ya kutekeleza mradi wa ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa kilovoti 132 kutoka Songea hadi Masasi kupitia Namtumbo, Tunduru na Nanyumbu umbali wa kilometa 395.

Mheshimiwa Naibu Spika, (TANESCO) pia inaendelea na taratibu za ujenzi wa Vituo vya kupoza umeme vya msongo wa kilovoti 132 kwenda 33 vya Namtumbo na Tunduru Mkoa wa Ruvuma, pamoja na vituo vya Nanyumbu na Masasi Mkoa wa Mtwara. Ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza ifikapo Desemba, 2022 na kukamilika mwezi Desemba, 2023 na gharama ya mradi inakadiriwa kuwa shilingi bilioni 132.7.