Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA Aliuliza: - Je Serikali inatumia mikakati gani kudhibiti mapato yatokanayo na gawio kutoka kwenye makampuni ambayo Serikali inamiliki hisa chini ya 50%?

Supplementary Question 1

MHE. JESCA D. KISHOA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante, pamoja na majibu ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuhakikisha uhalali wa magawio ambayo tunapewa kutoka kwenye makampuni haya Serikali haioni kama kuna haja ya ku-list share zake kwenye stock market ambako kule wanafanya scrutiny ya hali ya juu pamoja na kuweka hesabu wazi?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kwa maslahi mapana ya umma ni lini Serikali itaona ipo haja ya CAG kupewa mamlaka kisheria ya kuweza kufanya ukaguzi kwenye mashirika na makampuni hayo? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa maswali mazuri ambayo yanaelezea mpango mbadala wa kuona namna gani CAG anaweza akakagua mashirika haya ambayo Serikali ina hisa chache.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikianza na la kwanza la listing of shares nadhani kuna taratibu tu ambazo huwa tunafanya uchambuzi hata kwa mashirika haya ambayo Serikali ina hisa kubwa tunaangalia namna ambavyo yanaweza yakastahimili kwenye ushindani ule punde watakapokuwa wameshaweka hesabu zao zote zikiwa sawa, kwa sababu kuna implication zingine za viashiria vya performance za mashirika ambavyo vinatumika.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili la pili la CAG kuweza kukagua hata kwenye maeneo ambayo Serikali ina hisa chache nikiri tu kwamba hilo ni wazo jema na sisi kama Serikali tunaona tunapokwenda huenda kukawa na uhitaji huo kwa sababu utakubaliana na mimi kwamba hata juzi juzi tulibadilisha sheria kuweza kuiruhusu Serikali kuweka guarantee hata katika maeneo ambayo Serikali ina hisa chache, tukiwa tumeenda kwenye uchumi wa kisasa ama kwenye uwekezaji wa kisasa wa maeneo ambayo ni miradi mikubwa kama ilivyo kwenye bomba la mafuta.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa maana hiyo kwenye bomba la mafuta hata kama Serikali ina hisa chache lakini uwekezaji wake ambao Serikali inaweka unaweza ukawa mkubwa kuliko eneo ambalo Serikali ina hisa chache kwa maana hiyo kutakuwepo na justification ya kuona kwamba CAG anaenda kufanya ukaguzi kwenye maeneo ambayo Serikali imeweka uwekezaji na ni uwekezaji mkubwa licha ya kwamba inaweza ikawa na hisa chache.