Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 4 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 44 2021-09-03

Name

Jesca David Kishoa

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JESCA D. KISHOA Aliuliza: -

Je Serikali inatumia mikakati gani kudhibiti mapato yatokanayo na gawio kutoka kwenye makampuni ambayo Serikali inamiliki hisa chini ya 50%?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO Alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jesca David Kishoa, Mbunge Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina ambaye ndiye msimamizi wa uwekezaji wa Serikali katika Taasisi na Mashirika ya Umma pamoja na Kampuni ambazo Serikali ina hisa chache, inadhibiti mapato yatokanayo na gawio kwa kuhakikisha kuwa kila kampuni ina sera ya gawio, kurejea kwa mikataba ya mauzo ya hisa katika kuhakikisha maslahi ya Serikali yanalindwa pamoja na kufanya chambuzi za mara kwa mara kuhusu utendaji wa taasisi hizo. Aidha, Serikali inauwakilishi kwenye bodi za wakurugenzi wa kampuni ambapo pamoja na mambo mengine husimamia maslahi ya Serikali kwenye kampuni ikiwa ni pamoja na malipo ya gawio.

Mheshimiwa Naibu Spika, mikakati hii imeiwezesha Serikali kuongeza makusanyo yake ya gawio kutoka kampuni ambazo ina hisa chache kutoka shilingi bilioni 34.92 mwaka 2015/2016 hadi kufikia shilingi bilioni 155.10 mwaka 2020/2021.