Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA K.n.y. MHE. NG’WASI D. KAMANI Aliuliza:- Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka sasa wa kufanya masomo ya Ujasiriamalai na Usimamizi wa Fedha kuwa masomo ya lazima kwa kila mwanafunzi nchini kwa kuwa Elimu ya Ujasiriamali ni mbadala wa changamoto ya ajira kwa vijana?

Supplementary Question 1

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo majibu ya Serikali yameweza kukiri kwamba, mfumo wa sasa wa elimu bado haujakuwa suluhisho la vijana wengi wanaomaliza na kwenda kujiajiri wao wenyewe.

Je, ni lini hasa Serikali itakamilisha mchakato wa mabadiliko haya, ili tuweze kwenda na mfumo kama ambavyo Serikali imeweza kukiri kwamba, hatuko kwenye mfumo wa kidunia, hatujaweza kukimbizana nao?

Je, Serikali ni lini itakamilisha mchakato huo ili kuwasaidia vijana wengi wanaotoka kwenye shule waweze kwenda kujiajiri wao wenyewe? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi kwamba, sasa tuko katika mjadala wa kitaifa wa kuhakikisha kwamba, tunaboresha mitaala yetu hii, ili kuingiza stadi za kazi, lakini vilevile kuingiza mambo yote yanayoonekana ni muhimu kuhakikisha kwamba, tunajenga umahiri wa vijana wetu. Mchakato huo tumeanza na tumeanza katika Mkoa wa Dar es Salaam, lakini vilevile tulifanya mjadala mpana hapa Dodoma na tuna website ya kuhakikisha kwamba, tunakusanya maoni hayo.

Mheshimiwa Spika, tutaendelea na mchakato huu wa kukusanya maoni. Na ndani ya mwaka huu wa fedha tunakadiria au tunakusudia kuhakikisha mchakato huu uweze kukamilika, ili tuweze kupata mitaala ile ambayo nchi yetu inayohitaji. Ahsante.

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA K.n.y. MHE. NG’WASI D. KAMANI Aliuliza:- Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka sasa wa kufanya masomo ya Ujasiriamalai na Usimamizi wa Fedha kuwa masomo ya lazima kwa kila mwanafunzi nchini kwa kuwa Elimu ya Ujasiriamali ni mbadala wa changamoto ya ajira kwa vijana?

Supplementary Question 2

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kupata nafasi:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa sisi wakati tunasoma miaka ya 70 sekondari tulikuwa na mchepuo wa needle work na cookery.

Mheshimiwa Spika, naomba niwaambie Waheshimiwa Wabunge kwamba, kwa needle work niliyoisoma miaka ile ya 70 nimeweza kushona kibiashara mpaka leo nafanya hiyo kazi. Hivi Serikali kweli hamuoni ni muhimu sana kuwafanya akinamama waweze kupata kitu ambacho watakibeba mpaka wakiwa watu wazima?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Malecela, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Malecela, kama nilivyozungumza mwanzo kwamba, tuko kwenye mjadala, mjadala ambao utawahusisha vilevile Wabunge. Ninyi Waheshimiwa Wabunge ndio ambao mtaamua kwamba, vitu gani tuweke kwenye mitaala yetu kwa lengo la kuhakikisha tunatengeneza jamii, tunatengeneza kizazi ambacho kitakwenda kujitegemea katika nyanja hizo ambazo tunazihitaji.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, wakati huo utakapofika Waheshimiwa Wabunge tutaomba tupokee maoni yenu na sisi bila tatizo lolote tutaingiza kwenye mitaala hiyo, ili kuhakikisha tunatengeneza Taifa lenye kujitegemea. Ahsante.

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ambayo ameyatoa na niongeze tu dogo kwamba, pamoja na maboresho ambayo tunayafanya, lakini hata sasa somo la needle work na cookery linafanyika, lakini kwa shule chache.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nilikuwa nataka tu pia ifahamike hivyo kwamba, linaendelea kutolewa, lakini sio somo kwa wote. Kwa hiyo, tutazingatia kuona kuna umuhimu na tunakubaliana kwamba, kuna umuhimu wa kuhakikisha vijana wengi wa kitanzania wanapata ujuzi huo. Ahsante sana. (Makofi)