Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 2 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 28 2021-09-01

Name

Ng'wasi Damas Kamani

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ASIA A. HALAMGA K.n.y. MHE. NG’WASI D. KAMANI Aliuliza:-

Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka sasa wa kufanya masomo ya Ujasiriamalai na Usimamizi wa Fedha kuwa masomo ya lazima kwa kila mwanafunzi nchini kwa kuwa Elimu ya Ujasiriamali ni mbadala wa changamoto ya ajira kwa vijana?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA Alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ng’wasi Damas Kamani, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa kufundisha masomo ya ujasiriamali na usimamizi wa fedha ili kuwajengea wanafunzi stadi na ujuzi utakaowasaidia kukabiliana na changamoto mbalimbali katika jamii ikiwemo suala la ajira.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa masomo hayo yanafundishwa kuanzia ngazi ya elimu msingi na sekondari kama ifuatavyo: Shule za Msingi, Ujasiriamali na Usimamizi wa Fedha hufundishwa katika masomo ya stadi za kazi, maarifa ya jamii na hisabati. Katika ngazi za Shule ya Sekondari, masomo haya hufundishwa katika masomo ya Civics na General Studies ambayo husomwa na wanafuzni wote. Aidha, masomo hayo hufundishwa katika masomo chaguzi kama vile Book Keeping, Commerce, Economics, Accountancy, Home Economics, Mathematics na Agriculture.

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na zoezi la kuboresha mitaala na mihtasari ya masomo katika ngazi ya elimu ya awali, msingi na sekondari kwa lengo la kuandaa mitaala itakayokidhi mahitaji na mabadiliko ya kisiasa, kiuchumi, kijamii katika ulimwengu wa sasa.

Mheshimiwa Spika, katika hatua hii, Serikali itatilia mkazo mbinu tete na stadi za maisha hususan stadi za karne ya 21 ambazo ni fikra tunduizi, ubunifu, ushirikiano, uongozi na stadi za teknolojia habari na mawasiliano ili kuwajengea wanafunzi uwezo wa kukabiliana na mabadiliko mbalimbali yanayotokea katika jamii yetu na dunia kwa ujumla likiwemo suala la ajira. Ahsante. (Makofi)