Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA Aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa bandari kavu inayojengwa Katosho Kigoma?

Supplementary Question 1

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Spika, kwanza, nashukuru sana kwa majibu yaliyotolewa na Serikali na katika majibu hayo inaonekana kwamba imekadiriwa tani 500,000 ndiyo zitakazokuwa zinapita kwenye bandari hiyo kavu lakini mpaka sasa ni tani 200,000 tu, kwa hiyo, wanasema bandari haijazidiwa.

Mheshimiwa Spika, lakini jambo la msingi ambalo nilitaka Serikali ilifahamu ni kwamba kutokuongezeka kwa mizigo kumetokana na kukosekana kwa mabehewa ya mizigo na ubovu wa reli vitu ambavyo vinakwenda kutengenezwa katika bajeti ya mwaka huu. Je, Serikali haioni kama ni busara kwenda sambamba na kukamilisha bandari hiyo badala ya kusubiri bandari izidiwe wakati ile bandari kavu ya kuhifadhi makasha itakuwa haijakamilika?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA W. WAITARA): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilumbe Shabani Ng’enda, Mbunge wa Kigoma Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba shehena ilikuwa imepungua na mwaka huu wa fedha tunaongeza mabehewa na katika jibu la msingi utaona tayari fidia ya eneo hilo lote hekta 69 imeshafidiwa na mwaka wa fedha ujao tunaanza ujenzi. Kwa hiyo, kwa kadri tutakuwa tunapata fedha tutakuwa tunajenga kwa kadri ya mahitaji yanavyokua. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba bandari hii haitazidiwa na itajengwa kadri tutakapokuwa tunapata fedha. Kwa hiyo, asiwe na wasiwasi wowote ule, tunalifanyia kazi, ahsante.