Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka wakaguzi ili kuhakiki thamani ya fedha ya Shilingi bilioni 15 zilizotolewa na Serikali kwa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa ajili ya mradi wa maji wa Masukulu ambao unaonekana kujengwa chini ya kiwango?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA, Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Kwa majibu yaliyotolewa na Serikali, nilikuwa ninamuomba Mheshimiwa Waziri kwa kushirikiana na mimi pamoja na Madiwani wa Wilaya ya Rungwe aweze kufuatilia uhalali wa majibu waliyompatia, hilo swali la kwanza.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Kijiji cha Mpuguso Itula, Lukoba kinapata maji kutoka chanzo cha Kasyeto lakini, Kasyeto yenyewe ambayo inatoa chanzo cha maji wanakijiji wake hawapati maji. Je, ni lini Serikali itahakikisha watu hawa wa Kasyeto pamoja na Mpumbuli wanapata maji, maana wao ndiyo wanaotoa chanzo cha maji nao si wanufaika wa maji? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Mwakagenda kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa majibu ambayo Serikali imeweza kutoa hapa ni majibu yenye uhakika. Hata hivyo tutatuma timu yetu kwenda kufanya uhakiki wa kuona uhalali wa maelezo ya Mheshimiwa Mbunge. Vilevile kwa vijiji vya Mpuguso na vijiji jirani, na vile vijiji ambavyo chanzo cha maji kinatokea kama ilivyo ada ya Wizara ya Maji vijiji ambavyo vinatoa chanzo cha maji huwa ndio wanufaika namba moja.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo hili ninaendelea kutoa maelekezo kwa watendaji wote wa Wizara ya Maji na RUWASA, pamoja na Mamlaka kuhakikisha maeneo yote ambayo yanatoa vyanzo vya maji lazima wawe wanufaika namba moja.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka wakaguzi ili kuhakiki thamani ya fedha ya Shilingi bilioni 15 zilizotolewa na Serikali kwa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa ajili ya mradi wa maji wa Masukulu ambao unaonekana kujengwa chini ya kiwango?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Serikali imeweza kutoa fedha nyingi sana za walipa kodi masikini kwenda kwenye miradi ya maji, lakini uhalisia ni kwamba miradi mingi sana haitoi maji kwa ukamilifu au mingine haitoi maji kabisa. Ningependa kujua, ni lini Serikali itafanya ukaguzi kwenye miradi yote nchi nzima ambayo haitoi maji ili sasa iweze kutubainishia bayana ni miradi ipi kwa fedha kiasi gani zimewekezwa na haitoi maji kwa wananchi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Matiko kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli fedha nyingi zimeelekezwa katika miradi ya maji na ndiyo maana tatizo la maji linaendelea kupungua. Namna ambavyo tatizo lilikuwa huko awali ni tofauti na sasa hivi, na tayari sisi Wizara tunafanya kazi kwa makusudi kabisa usiku na mchana ili kuhakikisha kuona kwamba miradi yote ambayo haitoi maji itatoa maji. Tayari miradi ambayo ilikuwa ya muda mrefu haikuweza kutoa maji. Baadhi tayari inatoa maji na tayari watendaji wetu wanaendelea kufanya kazi. Tutahakikisha miradi yote ambayo maji hayatoki maji yatatoka bombani.

Name

Khadija Shaaban Taya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka wakaguzi ili kuhakiki thamani ya fedha ya Shilingi bilioni 15 zilizotolewa na Serikali kwa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa ajili ya mradi wa maji wa Masukulu ambao unaonekana kujengwa chini ya kiwango?

Supplementary Question 3

MHE. KHADIJA S. TAYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Kwa kuwa Serikali ilikuwa na nia njema sana ya sisi kuhamia Dodoma, na Dodoma sasa imekuwa ni sehemu ambayo ina mrundikano wa watu na maji pia yamekuwa hayatoshelezi. Je, ni lini Serikali itatekeleza ile adhma yake ya kuleta mradi wa Ziwa Victoria mpaka hapa Dodoma ili tuweze kupata maji hapa Dodoma?

Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nikushukuru sana. Kubwa ni kwamba tulishafanya kikao mimi pamoja na Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa wa Dodoma na ukiwa kama mwenyekiti. Juzi Mheshimiwa Rais alitoa maelekezo, na ameenda mbali zaidi ya kusema ukizingua, tutazinguana.

Mheshimiwa Spika, nikiwa kama Waziri wa Maji na timu yangu tumeshajipanga na tumeshafanya stadi tunahangaika kutafuta fedha…

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka wakaguzi ili kuhakiki thamani ya fedha ya Shilingi bilioni 15 zilizotolewa na Serikali kwa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa ajili ya mradi wa maji wa Masukulu ambao unaonekana kujengwa chini ya kiwango?

Supplementary Question 4

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa swali la msingi la Halmashauri ya Rungwe linafanana sana na tatizo la Halmashauri ya Rorya ambayo kwa 2015/ 2020, Serikali ilitupa zaidi ya bilioni 7.9 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji zaidi ya miradi 12, lakini mpaka sasa ninavyozungumza hakuna mradi ambao umetekelezwa kwa kiwango cha 100% na wakandarasi wameshalipwa fedha na hawapo site.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Mheshimiwa Waziri alifanya ziara mwezi wa kumi na mbili na akatoa maelekezo kwamba wakandarasi hao wakamatwe lakini mpaka leo ninavyozungumza hakuna mkandarasi aliyekamatwa badala yake kuna fedha inatoka kuja kukamilisha miradi ambayo kuna wakandarasi wamekula fedha.

Mheshimiwa Spika, swali langu ni, je, lini Serikali sasa itaona umuhimu wa kuleta wakaguzi kwenye Halmashauri ile ili kujiridhisha ile fedha bilioni 7.9 kwa miaka ile mitano imetumika vipi na yule ambaye kweli ametumia hizo fedha pasipo kutimiza wajibu wake achukuliwe hatua zinazo stahiki? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jafari Chege kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali ilitoa fedha nyingi sana kwa Halmashauri ya Rorya, na swali lake anahitaji kujua lini wakaguzi watapelekwa kuona namna gani wale ambao walikula fedha wanashuhulikiwa. Sisi kama Wizara tayari tumeunda timu yetu ambayo itazunguka majimbo yote kuona kwamba miradi ambayo fedha ilitoka na wakandarasi wakafanya janja janja basi wanakwenda kushughulikiwa na kama kuna mtumishi yeyote wa Serikali aliweza kujihusisha pamoja na hawa wakandarasi na yeye sheria itafuata mkondo wake.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nipende kumjibu Mheshimiwa Mbunge kwamba hivi karibuni watafika Rorya na wote ambao wanastahili kutumikia sheria basi sheria itafuata mkondo wake.

Name

Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA Aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka wakaguzi ili kuhakiki thamani ya fedha ya Shilingi bilioni 15 zilizotolewa na Serikali kwa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa ajili ya mradi wa maji wa Masukulu ambao unaonekana kujengwa chini ya kiwango?

Supplementary Question 5

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia fursa ya mimi kuuliza swali la nyongeza kwenye Wizara hii muhimu.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Chemba ni kati ya wilaya ambazo zinachangamoto kubwa sana ya maji. Nilitaka kujua tu Serikali, ni lini itawapatia maji wananchi wa vijiji; Chandama, Changamka, Babayo, Maziwa pamoja na Ovada?

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kunti kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa Wilaya ya Chemba pia taasisi yetu ambayo iko pale inaendelea kufanya jitihada kuona vijiji hivi ulivyovitaja vinapata maji mapema iwezekanavyo. Naomba mtupe muda tuweze kufanya kazi, siku si nyingi kabla ya mwaka huu wa fedha tayari tutapunguza idadi ya vijiji ambavyo havina maji kwa Chemba.