Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 5 Water and Irrigation Wizara ya Maji 36 2021-04-08

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA Aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itapeleka wakaguzi ili kuhakiki thamani ya fedha ya Shilingi bilioni 15 zilizotolewa na Serikali kwa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe kwa ajili ya mradi wa maji wa Masukulu ambao unaonekana kujengwa chini ya kiwango?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI MAJI: Mheshimiwa Spika; kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sophia Hebron Mwakagenda Mbunge wa Rungwe Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika; ni kweli Serikali kupitia Wizara ya Maji ilitekeleza mradi wa Maji wa Masukulu katika Wilaya ya Rungwe ambao ulitenga kuhudumia vijiji viwili vya Ijigha na Masukulu kwa gharama ya Shilingi milioni 335.6 na si shilingi bilioni 15 kama ilivyoelezwa na Mheshimiwa Mbunge. Mradi huo ulihusisha ujenzi wa chanzo, tanki lenye ujazo wa lita 90,000 na vituo 13 vya kuchotea maji vimekamilika na vinatoa huduma kwa wananchi wapatao 3,706.

Mheshimiwa Spika; katika kuhakikisha vijiji vya Ijigha na Masukulu vinapata huduma ya maji safi, salama na yenye kutosheleza; RUWASA Wilaya ya Rungwe inatumia chanzo cha maji cha Mto Mbaka ambacho kina cha maji kinatoa maji ya uhakika na tayari mradi huo umewekwa kwenye mpango wa bajeti ya RUWASA ya mwaka 2021/2022.